Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, February 22, 2015

UKURASA WA 53; Hakuna Kinachodumu Milele…

Moja ya siri kubwa unayopaswa kuijua ili kupata uhuru kwenye maisha ni kwamba hakuna kinachodumu milele.

Kama vile ambavyo sisi binadamu hatutadumu milele, siku moja utafikia mwisho, utakufa. Ndivyo ilivyo kwa kila kitu kwenye maisha, kuna wakati kitafika mwisho.

SOMA; Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..

Matatizo uliyonayo hayatadumu milele, kuna wakati yatafika mwisho, labda wewe mwenyewe uamue kutafuta matatizo mengine tena.

Hata kazi unayofanya sasa haitadumu milele, kuna siku itafika mwisho, utafukuzwa, kupunguzwa au kustaafu.

Biashara unayofanya sasa, hautaendelea kuifanya hivyo hivyo milele. Mambo yatabadilika na kama wewe hutabadilika utaachwa nyuma.

Mafanikio uliyonayo sasa hayatadumu milele, unahitaji kujifunz ambinu za kuendelea kuyaongeza kila siku.

Kwa kujua kwamba hakuna kidumucho milele, unaweza kujiandaa kwa nyakati ambazo ulichonacho sasa hakitakuwepo. Kushindwa kujiandaa ndio unajikuta kwenye wakati mgumu, kwenye matatizo makubwa.

SOMA; Ukurasa Wa 03; KIFO…(Umuhimu Wake Na Jinsi Unavyoweza Kukitumia Kufikia Mafanikio)

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba hakuna kidumucho milele, kila kitu kina mwanzo na mwisho wake. Nitajiandaa vizuri kwa vile vitu ambavyo nahitaji kuendelea kuwa navyo ili visiondoke na nikabaki na matatizo. Pia nitahakikisha vile nisivyotaka vinafika mwisho wake na sivitafuti tena.

Tukutane kwenye ukurasa wa 54 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment