Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, February 1, 2015

Ni Muda Unaenda Haraka Au Wewe Unaenda Taratibu?

Kufumba na kufumbua mwezi wa kwanza hatunao tena...
Tuko mwezi wa pili na siku sio nyingi tutauanza mwezi wa tatu.
Ni majuzi tu tulikuwa tunasherekea mwaka mpya, sasa hivi ni kama umechakaa.
Muda unakwenda haraka eh?
Hiki ndio kila mtu anachosema, kwamba muda unakwenda haraka sana.
Lakini je ni kweli?
Ni kweli muda unakwenda haraka au sisi tunakwenda taratibu?
Kipimo cha muda tunachotumia ni kile kile ambacho tumetumia miaka mingi iliyopita.
Iwe ni kwa kutumia saa, machweo na mawio na hata mzunguko wa mwezi. Vyote hivi havbijabadilika.
Ila sisi tunaona mabadiliko, muda unakwenda haraka sana.
Kwa dhana hii ya kwamba vipimo vyetu vya muda havijabadilika, ni dhahiri kamba sisi ndio tunakwenda taratibu.
Na kama tusipogundua mapema tutazidi kubaki nyuma.
Tufanye hima, muda hautusubiri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment