Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, February 23, 2015

UKURASA WA 54; Kufa MTUPU….

Moja ya njia zitakazokuwezesha kufanya kazi iliyobora kwa wakati ambao bado unaishi hapa duniani ni kupanga kufa MTUPU.

Kwa lugha ya kiingereza tunasema DIE EMPTY.

Kila mmoja wetu amezaliwa na mziki mzuri sana ambao upo ndani yake. Lakini ni wachache sana ambao wanaweza kuimba mziki huu. Na ninaposema mziki simaanishi mziki wa kuimba bali lile jambo ambalo uko bora kuliko mambo mengine yote.

SOMA; Njia TATU Za Kufanya Moto Wa Ujasiriamali Uendelee Kuwaka Kwenye Nafsi Yako…

Hiki ndio kimejaa ndani yako na unatakiw akukitoa bila ya choyo, bila ya kukibania. Kwa sababu huna sehemu nyingine ya kwenda kukitoa tena zaidi ya hapa duniani. Na huna wakati mwingine wa kukitoa zaidi ya leo, zaidi ya sasa.

Hakikisha unajikamua mpaka tone la mwisho la ubora wako. Kama umewahi kuona jinsi ambavyo mtu anakamua juisi ya miwa, ndivyo unavyotakiwa kufanya kwako binafsi.

Na uzuri wetu binadamu ni kwamba jinsi unavyojikamua ndivyo unavyozidi kutoa ubora zaidi.

SOMA; Hatua TANO Za Kuongeza Uzalishaji Wako Ili Kufikia Mafanikio.

Usikubali kufanya tu kazi ya kawaida wakati unaweza kuwa bora zaidi. Usikubali tu kufanya biashara ya kawaida wakati unaweza kuwa bora sana. Mara zote pigania kuwa bora, kwa sababu una uwezo huo na amua kufa MTUPU, uache ubora wote kwa faida ya dunia na vizazi vijavyo.

TAMKO LA LEO;

Naamua kufa MTUPU. Sitaibadia dunia hii ubora ambao upo ndani yangu. Sitaki kuondoka na mziki wangu ukiwa haujachezwa hapa duniani. Chochote ninachofanya nitakifanya kwa ubora wa hali ya juu sana, kwa ubora wa kiwango cha daraja la kwanza. Kama ambavyo haijawahi kufanywa na mwingine yeyote duniani. Kwa sababu mimi ni wa pekee.

Tukutane kwenye ukurasa wa 55 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA

SOMA; Weka Pamoja Vitu Hivi Vitatu Na Tayari Wewe Ni Mjasiriamali Mwenye Mafanikio Makubwa.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment