Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, February 18, 2015

UKURASA WA 49; Uelekeo Ni Muhimu Kuliko Mwendo Kasi..

Kama hujui unakokwenda, kuongeza mwendo hakutakufikisha unakotaka kufika.

Kuongeza mwendo kutazidi kukupoteza, kukupeleka mbali zaidi na huenda ukawa mbali zaidi na unakotaka kufika.

Hivyo jukumu lako kubwa kwenye maisha sio kuongeza mwendo bali kujua kwanza unakokwenda ni wapi.

SOMA; Sababu 5 Kwa Nini Ni Marufuku Wewe Kukata Tamaa.

Ukishajua unakokwenda ni wapi, hapo ndio unapoweza kuongeza mwendo na ukaweza kufika pale.

Ila kwenye maisha watu wengi wanaongeza mwendo bila ya kujua uelekeo wao na hivyo kujikuta wanapotea zaidi.

Unaanza kufanya kazi ambayo hujaiwekea malengo, unapofika katikati unapotea. Unapoongeza juhudi na maarifa kwenye kazi hiyo unazidi kupotea, unazidi kuharibu.

SOMA; Mambo 5 Muhimu Ya Kufanya Kabla Hujalala Leo.

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba uelekeo ni muhimu zaidi kuliko mwendo kasi. Mara zote nitahakikisha nipo kwenye uelekeo sahihi wa kufikia malengo yangu kabla sijaongeza mwendo. Maana kwa kuongeza mwendo bila ya kujua uelekeo ni kuendelea kupotea zaidi.

Tukutane kwenye ukurasa wa 50 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Biashara 5 Unazoweza Kuanza Kufanya Bila Ya Kuwa Na Mtaji.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment