Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, February 27, 2015

UKURASA WA 58; Usikubali Kubeba Matatizo Ya Mtu.

Unaruhusiwa kumsaidia mtu, na tunahitaji sana kusaidiana ili tuweze kufikia mafanikio.

Lakini kama njia yako ya kumsaidia mtu ni kuyabeba matatizo yake basi unajiandaa kushindwa. Kuna watu wengi sana ambao unahitaji kuwasaidia kiasi kwamba ukitaka kubeba matatizo yao yote maisha yako yatakuwa hovyo sana.

Unapomsaidia mtu, hakikisha maisha yako wewe hayawi hovyo kuliko ya yule ambaye unamsaidia, ikiwa hivyo msaada wako hautakuwa na maana.

SOMA; NENO LA LEO; Huwezi Kuanguka Kama Hutafanya Hivi.

Msaidie mtu kujisaidia mwenyewe, na hii ndio njia bora kabisa. Maana msaada wa mtu unatoka ndani yake kama ataelekezwa na kuongozwa. Ila kama wewe ndio unataka uyabebe matatizo yote utajikuta kwenye wakati mgumu sana.

Kwa mfano una ndugu yako ambaye ni mlevi sana na kila akipata fedha analewa mpaka anakuwa hajitambui. Halafu akimaliza fedha zote anakuwa na maisha magumu sana kiasi cha kutia huruma. Je ukitaka kumsaidia utampa fedha? Fanya hivyo kununua matatizo zaidi, maana kwanza atakutegemea wewe moja kwa moja wka fedha na utaongeza tabia yake ya ulevi. Fikiria njia bora zaidi.

SOMA; NENO LA LEO; Hiki Ndio Chanzo Cha Furaha.

Hivyo usikimbilie tu kutoa msaada hakikisha msaada huo unakuwa wa maana kwa watu wote wanaohusika.

TAMKO LA LEO;

Niko tayari kuwasaidia watu wanaonizunguka ila sipo tayari kubeba matatizo yao. Kwa kuwa kama na mimi nitakuwa kwenye matatizo hakuna atakayeweza kumsaidia mwenzake. Nitahakikisha namsaidia mtu kujisaidia mwenyewe.

Tukutane kwenye ukurasa wa 59 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; KURASA YA 01; Maisha Unayoishi Ni Yako.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment