Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, February 1, 2015

UKURASA WA 32; Mambo Yanapokuwa Magumu…

Mambo yanapokuwa magumu, huu ni uhakika, yatakuwa magumu, unafanya nini?

Umeshaweka malengo na mipango yako vizuri.

Umeshajitoa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Umekazana kwa juhudi zako zote, umekuwa mvumilivu lakini mambo hayae kabisa, huoni mabadiliko yoyote.

Unafanya nini? Unakubali kwamba lengo hili haliwezekani na hivyo unaachana nalo? Kosa kubwa sana.

SOMA; Jambo Muhimu La Kufanya Leo Jumapili Usiku.

Hata mambo yawe magumu kiasi gani, usibadili lengo, bali badili baadhi ya mipango au njia ambazo unaona hazizai matunda.

Ukibadili lengo umekwisha, maana hata ukiweka lengo jingine yatajirudia hayo hayo.

Hivyo usibadili lengo, bali badili baadhi ya mbinu au mipango ambayo haionekani kuleta matokeo unayotaka.

TAMKO LA LEO;

Mambo yatakapokuwa magumu sitabadili lengo bali nitabadili mipango na mbinu ambazo hazileti mabadiliko mazuri. Najua nikibadili lengo langu nitakuwa nimejiondoa mwenyewe kwenye safari ya mafanikio.

Tukutane kwenye ukurasa wa 33 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Mambo Matano Ambayo Viongozi Bora Hufanya Kila Siku.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment