Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, February 2, 2015

UKURASA WA 33; Tengeneza Mtandao Wako Wa Mafanikio.

Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kufanya kila kitu yeye mwenyewe. Na hata kwenye mafanikio, hakuna mtu ambaye anaweza kusema amefikia mafanikio yeye mwenyewe kwa nguvu zake mwenyewe tu.

Ili kufikia mafanikio unahitaji ushirikiano wa watu wengi sana.

Ni muhimu sana kutengeneza mtandao ambao utakufikisha kwenye mafanikio. Shirikiana na watu ambao wana malengo ya kufikia mafanikio kama wewe.

Kumbuka mafanikio yako ni wastani wa mafanikio ya watu watano unaokuwa nao kwa muda mrefu. Hivyo kama unashirikiana na watu ambao hawana njaa ya mafanikio na wewe hutofikia mafanikio.

SOMA; SIRI 50 ZA MAFANIKIO.

Mafanikio yako yanategemea ni watu wangapi wenye mafanikio wanaokuzunguka zaidi ya kile unachofanya.

TAMKO LA LEO;

Najua ya kwamba mafanikio yangu yanategemea sana wale wanaonizunguka. Hivyo kama nataka kufanikiwa zaidi inabidi nizungukwe na wale ambao wamefanikiwa zaidi. Nitajenga mtandao mzuri utakaoniwezesha mimi kufikia mafanikio.

Tukutane kwenye ukurasa wa 34 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment