Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, February 17, 2015

UKURASA WA 48; Ni Marufuku Kubadili Lengo…

Kuna usemi unakwenda, ujinga ni kufanya jambo lile lile na kw anjia ile ile halafu ukategemea majibu tofauti.

Yaani kama unalima shamba lako na unapanda mbegu fulani na kutumia mbolea fulani na ukanyeshea vizuri, kama usipopata mazao mazuri, hata wakati mwingine ukilima hivyo hivyo utapata kama ulivyopata.

SOMA; UKURASA WA 20; Geuza Changamoto Kuwa Fursa.

Kama unafanya kile kitu ulichopanga lakini bado hupati majibu unayotarajia, kuendelea kufanya hivyo hivyo ni vigumu kupata kile unachotaka. Kwa maana hiyo ni kwamba kuna vitu ambavyo unatakiwa kubadili.

Ila ni marufuku kubadili lengo lako kuu unalofanyia kazi kwenye maisha. Badili njia unazotumia kufikia lengo lako, ila usibadili lengo.

Kukubali kubadili lengo maana yake umekubali kushindwa na hata utakapokwenda kuanza lengo jingine itakuwa rahisi kwako kuliacha pia.

Changamoto hazikosekani kwenye jambo lolote unalotaka kufanya, ila ukikubali zikufanye uache kile unachotaka utashindwa katika kila jambo unalofanya kwenye maisha yako.

SOMA; UKURASA WA 42; Usitafute Sababu, Chukua Hatua…

TAMKO LA LEO.

Najua kwamba kuna wakati mambo hayatakwenda kama nilivyopanga. Katika wakati huu nitabadili mbinu ninazotumia, ila sitabadili lengo langu kubwa kwenye maisha.

Tukutane kwenye ukurasa wa 49 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment