Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, February 12, 2015

UKURASA WA 43; Ushauri Wa Bure Una Gharama Kubwa.

Ushauri wa bure hauna gharama mpaka pale utakapoanza kuutumia.

Siku hizi kila mtu anajua kutoa ushauri, kuwa makini sana kabla hujatumia ushauri wowote unaopewa. Hasa ushauri unaotolewa na kila mtu.

Kuna maneno rahisi ya mtaani utasikia biashara fulani inalipa kweli, fulani kaanza kuifanya na sasa hivi yuko vizuri. Au utasikia kilimo fulani kinalipa kweli, watu wanaofanya wananufaika sana.

SOMA; Njia TATU Za Kufanya Moto Wa Ujasiriamali Uendelee Kuwaka Kwenye Nafsi Yako…

Mara nyingi utakuta wanaokupa ushauri wa aina hii wala hawafanyi hiko wanachokushauri.

Utakuja kujua ukweli pale unapojiingiza kwenye kitu hiko kinachoshauriwa, utakutana na changamoto ambazo hukuambiwa na kama hutakuwa imara unaweza kukata tamaa.

Kabla ya kufanyia kazi ushauri wote unaopewa, fanya utafiti wa kutosha, jua changamoto na vikwazo utakavyokutana navyo na unapoamua kuingia ingia moja kwa moja ukiwa na lengo moja tu, KUSHINDA.

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba ushauri unaotolewa na kila mtu sio ushauri mzuri sana kuufuata. Kabla sijafuata ushauri wowote ninaopewa, hasa wa bure, nitafanya utafiti ili nijue kwa undani kila kinachoendelea. Na nitakapoamua kufanyia kazi ushauri huo, sitarudi nyuma.

Tukutane kwenye ukurasa wa 44 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA

SOMA; Hatua TANO Za Kuongeza Uzalishaji Wako Ili Kufikia Mafanikio.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment