Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, February 16, 2015

NENO LA LEO; Faida Tatu Za Kazi…

“Work spares us from three evils: boredom, vice, and need”. Voltaire

Kazi inatuepusha na mambo matatu mabaya; kuchoka kwa kutofanya lolote, maovu na mahitaji.

Unaweza kuona kama kazi ni kitu kibaya sana ambacho kinakutesa.

Na wakati mwingine kutamani kwamba hata kazi zisingekuwepo.

Ila jiulize kama usingekuwa na kazi, usingechoka tu kukaa bila kufanya chochote?

SOMA; Sifa TATU Unazohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Je ungepataje mahitaji yako? Usingeshawishika kuiba au kuchukua vya wengine ili utimize mahitaji yako?

Kazi ni kitu kizuri sana ambacho tunatakiwa kukipenda.

Kwa sababu kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ndio msingi wa maendeleo na mafanikio.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Tabia Mbaya KUMI(10) Zinazopunguza Ufanisi Wako.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment