Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, March 29, 2015

UKURASA WA 88; Usinunue Matatizo Ya Watu.

Binadamu ni viumbe wa kujumuika, yaani tunaishi vizuri kwenye jamii, kwa kusaidiana hapa na pale.

Lakini katika kusaidiana huku kuna wakati ambapo tunatoa msaada ambao unatuumiza sana sisi na pia haumsaidii sana yule ambaye tunampatia.

Msaada huu ni pale ambapo unanunua matatizo yya mtu.

SOMA; Tabia Hizi Zitakusaidia Sana Kufikia Malengo Yako Kwa Haraka.

Unanunuaje matatizo ya watu?

Mtu anakuwa na tatizo, ambapo unashawishika kulitatua lakini katika kulitatua na wewe unaingia kwenye matatizo au hali yako inakuwa mbaya kuliko ilivyokuwa mwanzo. Unajikuta na wewe unaingia kwenye huzuni, unaanza kuona tatizo lile kama ni lako moja kwa moja.

Kama utafanya hivi kwa matatizo ya watu wengi, ni vigumu sana kuweza kuwa na maisha yenye furaha.

SOMA; Matatizo Yote Kwenye Maisha Yako Yanatokana Na Kitu Hiki.

Sikiliza matatizo ya watu, toa msaada kama unaweza, ila usizame moja kw amoja kwenye tatizo hilo. Kwa kufanya hivyo unakuwa umenunua tatizona litakusumbua sana wewe. Na pia kama huwezi kusaidia tatizo la mtu usiondoke nalo na likaendelea kukusumbua. Tambua ya kwmaba kila mtu ana matatizo yake na huwezi kutatua matatizo ya kila mtu.

Kwa hili haimaanishi kwmaba hujali matatizo ya watu, ila hubebi matatizo hayo na kuyafanya sehemu ya maisha yako. Wewe mwenyewe una matatizo yako yanayokusumbua, pambana na hayo kwanza.

SOMA; Jinsi Ya Kujijengea Uwezo Wa Kujiamini

TAMKO LA LEO;

Kuanzia sasa sitanunua tena matatizo ya watu. Sitachukua matatizo ya watu na kuyafanya sehemu ya maisha yangu. Nitasikiliza matatizo hayo na kama nitaweza kusaidia nitafanya hivyo, kama siwezi nitakiri kwamba siwezi na sitakubali nimezwe na matatizo haya.

Tukutane kwenye ukurasa wa 89 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment