Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, March 21, 2015

NENO LA LEO; Umuhimu Wa Kuchukua Hatari.

“Risk anything! Care no more for the opinion of others ... Do the hardest thing on earth for you. Act for yourself. Face the truth." ― Katherine Mansfield,

Kuchukua hatari ndio kila kitu. Usijali maoni ya wengine… Fanya vitu ambavyo ni vigumu sana kwako. Fanya mambo yako. Ukabili ukweli.

Kuna wakati mtu unaogopa kuchukua maamuzi ukiona kwamba ni maamuzi ya hatari sana kwako. Nikuambie kwamba maamuzi ya hatari ndio yanayoweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye maisha yako.

Kuna wakati ambao unaacha kufanya mambo magumu, unafanya mambo ambayo ni rahisi kwako. Nikuambie kwamba mambo magumu ndio yatakayokuletea manufaa makubwa kwenye maisha yako, yafanye hayo. Hakuna kitu rahisi.

SOMA; TAFAKARI YA LEO; Urefu Wa Muda Sio Mrefu.

Ukisikiliza maneno ya kila mtu, hutafanya jambo lolote kubwa kwenye maisha yako, maana watu hawakosi la kusema, hata kama ungefanya nini.

Fanya mambo yako, ukabili ukweli. Hakuna kinachoweza kuupinga ukweli, hata ukiukwepa kuna siku mambo yote yatakuwa wazi.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuwa Jasiri Na Kufanya Mambo Makubwa Zaidi Ya Unavyofikiria. ( 2)

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment