Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, March 23, 2015

UKURASA WA 82; Mambo Madogo Ndio Muhimu Sana.

Wakati unafikiria kuhusu mafanikio kwenye maisha unafikiria mambo makubwa sana.

Kama unafikiria kuhusu fedha unafikiria mamilioni na mabilioni.

Kama unafikiria kuhusu nyumba unafikiria hekalu, au nyumba kubwa sana yenye kila kitu.

Kama unafikiria usafiri unafikiria magari mengi na ya kifahari.

SOMA; KITABU; Jinsi Ya Kufaidika Na Mabadiliko Yanayotokea Kwenye Maisha.

Mambo yote haya ni mazuri sana na hakuna asiyependa vitu vizuri.

Ila ukweli unakuja kwamba, mambo madogo ndio yanayojenga maisha yetu. Yaani mambo madogo madogo ndio yana athari kubwa sana kwenye maisha tunayoishi.

Sio milioni mia moja au bilioni moja itakayokupa wewe uhuru wa kifedha, bali unawezaje kuitumia shilingi elfu moja vizuri, ikatimiza mahitaji yako na ukaweza kuweka akiba kidogo.

Sio jumba kubwa sana ambalo litaweza kukuletea furaha kwenye maisha, bali ni maisha gani unayoishi kwenye nyumba yoyote uliyopo sasa. Kama ni maisha ya amani na upendo yatakusukuma wewe kufikia jumba hilo kubwa hata kama unaanzia kwenye chumba kimoja.

SOMA; Haya Ndio Mapinduzi Makubwa Tunayohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Kilimo.

Vitu hivi vidogo vidogo ukiweza kuvizingatia vitakuletea mafanikio makubwa. Ukishindwa kuvizingatia maisha yako yatakuwa hovyo hata kama ungekuwa na vitu vikubwa kiasi gani.

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba vitu vidogo ndio muhimu sana kwenye maisha, ndio vinapelekea mambo makubwa kuwa muhimu kwetu. Nitaendelea kuzingatia mambo haya madogo ili maisha yangu yawe bora zaidi kila siku.

Tukutane kwenye ukurasa wa 83 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment