Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, March 20, 2015

NENO LA LEO; Sio Lazima Ufanye Maamuzi Sahihi.

“I do not believe in taking the right decision, I take a decision and make it right.” ― Muhammad Ali Jinnah

Siamini kwenye kufanya maamuzi sahihi, nafanya maamuzi kisha nayafanya yawe sahihi.

Kuna wakati ambao unaacha kufanya maamuzi kwa sababu huna uhakika kama maamuzi hayo yatakuwa sahihi au la. Au wakati mwingine unajua kabisa kwamba maamuzi yako hayatakuwa sahihi, hivyo hufanyi maamuzi.

SOMA; UKURASA WA 78; Hiki Ndio Kitu Unachoweza Kufanya, Bila Ya Kujali Uwezo Wako.

Kwa kutofanya maamuzi unaweza kuona uko salama, lakini kama unataka kufikia mafanikio makubwa, hiki ni kikwazo kikubwa sana kwako. Ili kufikia mafanikio unatakiwa kufanya maamuzi mengi na wakati mwingine kwa haraka. Unahitaji kuchukua nafasi ambazo wakati mwingine ni hatari.

Badala ya kusubiri uwe na uhakika ndio ufanye maamuzi fanya maamuzi kisha yafanye yawe sahihi. Fanya maamuzi yoyote ambayo yatakupelekea kufikia lengo lako, kisha yafanye maamuzi hayo kuwa sahihi. Kwa njia hii utaweza kuvuka vikwazo vingi sana na kufikia mafanikio.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Fikra TANO Zinazoua Mafanikio Na Jinsi Ya Kuziepuka.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment