Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, March 23, 2015

Je Umepata Kitabu Chako?

Siku kadhaa zilizopita niliweka ujumbe ambao nilikuomba wewe kama msomaji uwatumie watu wa tano kwenye email zao.
Na pia niliahidi ukifanya hivyo nitakupa zawadi ya kitabu kinachohusu mabadiliko.
Watu wengi walitikia ombi lile na ujumbe ulitumwa kwa watu wengi sana.
Jana kitabu kilikamilika na wewe uliyetuma ujumbe kwa wengine ulikuwa wa kwanza kutumiwa.
Naandika hapa nikotaka kujua kama umepata kitabu ulichotumiwa.
Kitabu kimetumwa kwa watu 33 ambao waliitikia wito ule.
Kama ulituma ujumbe na hujapokea kitabu tafadhali nijulishe kupitia email makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Nakupenda na kukuheshimu sana wewe msomaji wangu hivyo napenda kutimiza kile ninachokuahidi.
Pia nitumie nafasi hii kutangaza kwamba zoezi la kutuma ujumbe ule na baadae kupewa zawadi limefungwa rasmi.
Ila nakuomba uendelee kutuma jumbe hizi nzuri kwa watu wako wa karibu na washauri kujiunga nasi. Usitake kupata mambo haya mazuri peke yako, tusambaze elimu hii ili iwafikie wengi zaidi.
Asante na nakutakia kila la kheri.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment