Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, March 21, 2015

UKURASA WA 80; Utabiri Mzuri Wa Kesho.

Je unahitaji mtu wa kukusaidia kuitabiri vizuri kesho yako? Huna haja ya kwenda kwa wapiga ramli au watabiri wa nyota, kwani mtabiri bora kabisa tayari upo nae hapo ulipo. Mtabiri huyo ni wewe mwenyewe.

Unafikiria kama biashara unayofanya itakuletea mafanikio makubwa baadae?

Unafikiria kama kazi unayofanya utadumu nayo kwa muda mrefu?

Yote haya hayahitaji wewe kwend akwa mtabiri anayesifika, yanahitaji wewe ufanye jambo moja tu, ishi vizuri leo.

SOMA; Kesho Jua Litachomoza Tena...

Kama ukiishi vizuri leo, unakuwa umefanya maandalizi ya kuishi vizuri kesho. Kama utafanya biashara yako vizuri leo, unakuwa umetengeneza mazingira mazuri ya kufanikiwa kwenye biashara yako kesho. Kama ukifanya kazi yako vizuri leo unakuwa umetengeneza mazingira mazuri ya kufanya kazi nzuri zaidi kesho.

Kila kitu kitakwenda vizuri kesho kama utafanya vizuri leo.

Hivyo badala ya kuhofu kwamba mambo yatakwendaje kesho, badala ya kupoteza muda kutafuta watabiri, tumia muda huo kuishi vizuri leo na utatengeneza mazingira mazuri ya kesho.

TAMKO LA LEO;

Najua ya kwamba mtabiri mzuri wa maisha yangu ya kesho nu mimi mwenyewe na jinsi ya kufanya utabiri huu ni kuishi vizuri leo, kufanya kilicho chema leo na kesho mambo yatakwenda vizuri. Sitapoteza muda kuhofu kesho itakuwaje au kutafuta mtu wa kunitabiria, nitatumia muda huo kufanya vizuri leo na nina hakika kesho mambo yatakuwa mazuri sana.

SOMA; Jinsi Ya Kuondokana Na Hofu Ya Kuongea Mbele Za Watu.

Tukutane kwenye ukurasa wa 81 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment