Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, March 30, 2015

UKURASA WA 89; Sheria Tatu Muhimu Za Kufanikiwa Kwenye Maisha.

Watu hupenda kusema kwamba maisha hayana kanuni, yaani hakuna kanuni moja ambayo kila mtu akiifuata basi atakuwa na uhakika wa kuwa na maisha anayotaka. Pamoja na hii kuwa kweli, bado kuna sheria mbalimbali ambazo kama ukizifuata maisha yako yanakuwa bora na inakuwa rahisi kwako kufikia mafanikio.

SOMA; Biashara Unayofanya Sasa, Au Utakayoanza Sasa Sio Biashara Utakayofanya Milele.

Leo tutaangalia sheria tatu za msingi na muhimu sana ili kuwa na maisha bora na yenye mafanikio.

Sheria ya kwanza; Kama hutakiendea kile unachotaka hutokipata. Kwa urahisi ni kwmaba kama unataka mafanikio, halafu hufanyi jambo lolote la kukuletea mafanikio unayotaka, hutayapata. Kama kuna kitu unakitaka kwenye maisha yako, kifanyie kazi, kitafute na utakipata.

SOMA; KITABU; Jinsi Ya Kufaidika Na Mabadiliko Yanayotokea Kwenye Maisha.

Sheria ya pili; Kama hutauliza, jibu ni hapana. Kama kuna kitu ambacho unataka kumuuliza mtu, halafu ukaogopa kuuliza basi jibu tayari unalo, ambalo ni hapana. Usisite au kuogopa kuuliza au kuomba chochote, kabla hujaomba jibu ni hapana, hivyo omba na jibu likiwa hapana, halibadilishi chochote na kama jibu likiwa ni ndio utapata unachotaka.

SOMA; Unapokuwa Tayari Kuingia Kwenye Ujasiriamali Fanya Vitu Hivi Vitano.

Sheria ya tatu; Kama hutapiga hatua kwenda mbele, utaendelea kubaki hapo ulipo. Kama hutabadilika, kama hutafanya chochote cha kukusogeza mbele, utaendelea kuwa hapo ulipo, utaendelea kuwa na maisha uliyonayo.

Fanyia kazi kile unachotaka, omba au uliza unachotaka, piga hatua kwenda mbele.

TAMKO LA LEO;

Kuanzia sasa nitafanyia akzi kile ninachotaka ili niweze kukipata, nitauliza au kuomba kile ninachotaka kwa sababu najua nisipofanya hivyo jibu ni hapana. Na pia nitapiga hatua kwenda mbele kwenye kila eneo la maisha yangu. Sitakubali kubaki hivi nilivyo, nataka kuwa bora zaidi.

Tukutane kwenye ukurasa wa 90 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment