Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, March 30, 2015

NENO LA LEO; Haya Ndio Mambo Matatu Yatakayokuletea Matokeo Ya Kushangaza.

“Extra miles, extensive preparation and exhaustive efforts usually show astonishing results.” ― Roopleen

Kwenda hatua ya ziada, kujiandaa vyema na kuweka juhudi kubwa mara zote kutakuletea matokeo makubwa na ya kushangaza.

Jambo lolote unalofanya kwenye maisha yako na ambalo unataka likufikishe kwenye mafanikio makubwa ni muhimu sana uweke mambo haya matatu muhimu.

Nenda hatua ya ziada, usifanye tu kile ambacho kila mtu anafanya. Weka ubunifu zaidi, kuwa wa tofauti, ogopa sana kuwa kawaida. Maana kuwa kawaida ni sumu kubwa ya mafanikio.

SOMA; Kitu Hiki KImoja Kitakufanya Ushindwe Kwenye Biashara.

Kuwa na maandalizi ya kutosha. Jiandae vizuri kwa jambo lolote unalofanya kwenye maisha yako. Kuna changamoto nyingi sana kwenye maisha hivyo kama huna maandalizi ni rahisi sana kukata tamaa. Ila maandalizi haya yasiwe kikwazo kwako kuanza, anza huku ukiendelea kujiandaa zaidi.

Weka juhudi kubwa. Juhidi ndio zinazleta mafanikio. Hata kama ungekuw ana mipango mizuri kiasi gani, kama hutaifanyia kazi na kama hutaweka juhudi kubwa, hakuna chochote kitakachobadilika kwenye maisha yako.

SOMA; Nilichojifunza Leo; Zoezi Moja Litakalobadili Maisha Yako Kabisa.

Nakutakia siku njema.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment