Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, March 23, 2015

NENO LA LEO; Huu Ndio Ufunguo Wa Maisha, Na Sio Elimu.

“The key to life is accepting challenges. Once someone stops doing this, he's dead.” ― Bette Davis

Ufunguo wa maisha ni kuzikubali changamoto. Mtu atakapoacha kuzikubali changamoto, amekufa.

Hakuna maisha ambayo hayana changamoto, kwa kifupi hakuna mtu ambaye hana matatizo. Ukiwa huna fedha unakuwa na matatizo, ukiwa na fedha unakuwa na matatizo.

Njia moja ya kuweza kupambana na changamoto unazokutana nazo, kutatua matatizo unayokutana nayo ni kuyakubali kwanza.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuwa Jasiri Na Kufanya Mambo Makubwa Zaidi Ya Unavyofikiria. ( 2)

Kubali kwamba changamoto hii ni yako. Kubali kwamba uko kwenye matatizo. Na unaweza kuanzia hapa kujua unawezaje kujinasua kwenye matatizo haya.

Unaposhindwa kukubali, au ukaanza kukimbia changamoto na matatizo, yanazidi kuwa mengi zaidi na yatakumeza mzima mzima.

Nakutakia siku njema.

SOMA; KITABU; Jinsi Ya Kufaidika Na Mabadiliko Yanayotokea Kwenye Maisha.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment