Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, March 31, 2015

UKURASA WA 90; Kila Sehemu Utakayokwenda Utawakuta Watu Hawa.

Mtu mmoja alikuwa amechoshwa na watu kwenye mji aliokuwa anaishi. Kutokana na kuchoshwa huku aliona sulhisho pekee ni kuhama mji ule maana watu wale walifanya maisha yake kuwa magumu sana.

Alichagua mji mmoja wa kwenda na kabla ya kuhamia mji ule alitaka kuchunguza kwanza watu wa mji ule wana tabia gani. Alikwenda kwa mzee mmoja mwenye busara na kumwambia kwamba anataka kuhamia mji ule ila anapenda kujua watu wa mji ule wakoje.

SOMA; Mabadiliko; Yalikuwepo, Yapo Na Yataendelea Kuwepo.

Mzee yule mwenye busara alimuuliza swali moja, huko unakotoka watu wa huko wakoje? Alimjibu kwamba wana roho mbaya, ni wabinafsi na wana majungu sana. Mzee yule alimjibu kwamba hata kwenye mji ule anaotaka kuhamia watu wana tabia hizo hizo.

Dhana kubwa hapa ni kwamba kama unaona watu ulionao ni wabaya, wana roho mbaya, wabinafsi na mengine mengi, sehemu yoyote utakayokwenda utakutana na watu wa aina hiyo. Popote unapokwenda utakutana na watu ambao umechagua kuwaona.

SOMA; USHAURI; Hii Ndio Changamoto Kubwa Inayokuzuia Wewe Kutatua Changamoto Zako.

Ukiona kwmaba watu ni wazuri, wana roho nzuri, wanapend akusaidia, hiko ndio utakachokiona kila sehemu utakayokwenda.

Ukweli ni kwamba tunapata kile ambacho tunatarajia. Hivyo kama tunatarajia kupata mazuri kutoka kwa watu tutayapata na kama tunatarajia kupata mabaya pia tutayapata.

TAMKO LA LEO;

Najua matatizo makubwa hayapo kwa watu ninaowaona bali yapo ndani yangu mwenyewe. Kila sehemu nitakayokwenda, nitakutana na watu ambao natarajia kukutana nao. Kubadili mtizamo wangu juu ya watu, kutanisaidia sana ili kuweza kuishi maisha ya furaha.

SOMA; Jinsi Ya Kujijengea Uwezo Wa Kujiamini

Tukutane kwenye ukurasa wa 91 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment