Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, April 22, 2015

UKURASA WA 112; Njia Kuu Mbili Za Kuishi.

Kuna njia kuu mbili za kuishi maisha yako hapa duniani.

Njia ya kwanza ni kuishi kama ambavyo watu wanataka wewe uishi. Ufanye yale ambayo watu wanakutegemea uyafanye hata kama sio yanayokufurahisha au sio muhimu kwako. Ufanye kile ambacho kila mtu anafanya hata kama huna msukumo wowote wa kufanya hivyo. Hii ndio njia ya kwanza ambayo asilimia 99 ya watu kwenye jamii yoyote wanaishi njia hii.

SOMA; Kabla Hujabadili Tabia Zako Badili Hiki Kwanza…

Njia ya pili ni kuishi kama vile ambavyo wewe mwenyewe unataka kuishi. Kufanya kile ambacho ni muhimu kwako na una msukumo wa ndani wa kukifanya. Kufanya kazi wka juhudi na maarifa ili kuweza kufikia ndoto zako kubwa, bila ya kujali wengine wanafanya nini au wanasema nini. Kutokujiwekea ukomo wa wapi unapoweza kufika na kuwajali wale wanaokujali. Hii ni njia ya pili ambayo asilimia 1 ya watu kwenye jamii yoyote wanaishi njia hii.

Umechagua kuishi njia ipi? Huo ni uchaguzi wako. Kama hujachagua au hujui uchaguzi wako ni sahihi au la, nikukumbushe kwamba hii asilimia 1 wanaoishi maisha kwa njia ya pili, ndio wanaofikia mafanikio makubwa sana, wanaokuwa na furaha kwenye maisha yao na ambao hawana majuto kwenye maisha yao.

SOMA; Kama Huwezi Kufanya Miaka 50 Acha..

TAMKO LA LEO;

Najua maisha ni kuchagua, na kuna njia mbili za kuweza kuishi maisha yangu. Mimi nachagua kuishi njia ya ______________ na nitafanya mambo _____________ ili kuhakikisha maisha yangu yanakwenda vile nilivyopanga. (Jaza sehemu iliyoachwa wazi)

Tukutane kwenye ukurasa wa 113 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment