Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, April 7, 2015

Faida kumi za kuwa na MAONO kama nilivyojifunza kwenye kitabu THE PRINCIPLES AND POWER OF VISION.

Rafiki yangu Meshack Maganga​​ alinipa zawadi ya kitabu hiki. Aliniambia ni kitabu kizuri sana. Nikawa na shauku kubwa ya kukisoma na hatimaye nimekisoma na kwa kweli ni kitabu ambacho sijui kwa nini nimechelewa kukisoma. Ni kitabu chenye misingi yote ya kukuwezesha kufikia kile unachotaka kwenye maisha. Na hata kama hukijui basi utapata mwanga na utajua uliletwa duniani kufanya nini.
Kwa ufupi sana nikushirikishe mambo kumi muhimu kuhusu MAONO...
1. Kama hakuna MAONO watu wanaangamia.
2. Kesho yako haipo mbele yako, ipo ndani yako.
3. Unaweza kuwa unaona lakini huna maono.
4. Hukuzaliwa ili ufuate mbio za panga, shule - kazi - kuoa/kuolewa - watoto - kubadilu kazi - kustaafu - kufa. Maisha ni zaidi ya hapo.
5. Mtu masikini kuliko wote duniani ni mtu ambaye hana MAONO.
6. Mtu aliyevurugwa kuliko wote duniani ni yule mwenye ndoto ila hajui afikieje ndoto zako.
7. Haijalishi ni jambo dogo kiasi gani unafanya, kama utaweka moyo wako wote na maisha yako yote kwenye jambo hilo halitasahaulika kamwe.
8. Kama upo tayari kuweka nguvu zako zote kwenye kitu, hakuna anayeweza kukuzuia wewe kufikia mafanikio.
9. Haijalishi dunia ni kubwa kiasi gani, kuna sehemu yako kama utajua zawadi iliyopo ndani yako.
10. ELIMU SIO UFUNGUO WA MAISHA.(nimeiweka hii kwa herufi kubwa kama msisitizo)
Hiki nilichokushirikisha hapa ni punje tu ya mambo mengi utakayojifunza kwenye kitabu hiki. Kama hujakisoma nakusihi sana ukisome. Na kama huna mpango wa kusoma kitabu chochote kwenye maisha yako soma kitabu hiki tu basi. Utapata hazina kubwa sana ya kubadili na kuboresha maisha yako.
Kitabu kinapatikana house of wisdom bookshop nhc house, posta dar. Na bei yake ni ths 26,000/= tu.
Meshack anasema GO BIG OR GO HOME, na mimi naongeza kwamba BEFORE YOU GO HOME READ THIS BOOK, YOU MAY CHANGE YOUR MIND AND GO BIG.
TUPO PAMOJA.
www.amkamtanzania.com

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment