Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, April 17, 2015

NENO LA LEO; Unachotakiwa Kusema Na Unachotakiwa Kufanya.

I say what I want to say and do what I want to do. There's no in between. People will either love you for it or hate you for it. –Eminem

Nasema kile ninachotaka kusema na nafanya kile ninachotaka kufanya. Hakuna kuwa kati kati(vugu vugu). Watu watakupenda au kukuchukia kw akile unachosema na kufanya.

SOMA; Barua Ya Wazi Kwa Vijana Wanaotafuta Ajira. Soma Hapa Uone Fursa Unazoweza Kutumia.

Usiseme kitu kwa sababu unataka kuwafurahisha watu. Usifanye kitu kwa ajili ya kuwafurahisha watu. Unaweza kuwafurahisha wachache ila pia utawachukiza wengine.

Kama watu watakuchukia kwa jambo ambalo hata wewe hulipendi, maisha yako yanaweza kuwa magumu zaidi.

Ni bora ufanye kile unachotaka kufanya, sema kile unachotaka kusema. Kuna ambao watakupenda kwa hilo na watakupa moyo wa kufanya zaidi. Na kuna ambao watakuchukuia na kukupinga kwa hilo, hawa hawatakusumbua kwa sababu kile ulichosema au kufanya ndio unachopenda au kujali.

Kitu kinapokuwa na maana kwako na kama sio kinyume na sheria na taratibu basi usihofu kuhusu wachache watakaokupinga.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Siri Za Kuwa Mjasiriamali Bora Na Kufikia Mafanikio Makubwa.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment