Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, April 10, 2015

NENO LA LEO; Kinachofanya Maisha Yawezekane Na kinachoyafanya Yawe Rahisi.

Faith makes all things possible... love makes all things easy. -Dwight L. Moody

Imani inafanya kila kitu kiwezekane…. mapenzi(upendo) unafanya kila kitu kiwe rahisi.

Kama huna imani utaona kila kitu hakiwezekani hasa kwenye dunia hii ambayo imejaa kila aina ya changamoto, ni imani pekee itakayokuwezesha wewe kuendelea na mapambano licha ya kukutana na vikwazo. Amini kwamba unaweza, amini kwamba inawezekana na hakuna kitakachokuzuia kupata kile unachotaka.

SOMA; Huu Ndio Mtaji Mkubwa Ambao Tayari Unao.

Kama hakuna upendo, hakuna mapenzi maisha yatakuwa magumu sana. Upendo unatufanya tuweze kuwathamini wengine na wao kututhamini pia. Ni katika njia hii tunaweza kusaidiana na kuyafanya maisha kuwa rahisi sana. Mpende kila anayekuzunguka, jipende wewe mwenyewe na kubali pale wengine wanapokupenda. Hii ni zawadi pekee kwenye maisha ambayo haiangalii una nini, bali inakuangalia wewe kama wewe.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Hiki Ndio Kitu Kitakachokuletea Mafanikio Ambacho Tayari Unacho.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment