Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, April 18, 2015

UKURASA WA 108; Njia Ya Uhakika Ya Kuondokana Na Hofu.

Hofu ni kikwazo kikubwa kwa wengi kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yao.

Kama isingekuwa hifu leo hii ungekuwa mbali sana kuliko ulivyo sasa. Ndio nina uhakika kwa sababu wote tumekulia kwenye jamii ambazo zinatujaza sana hofu.

SOMA; Tumia Sheria Ya Mara 2, Mara 3 Kwenye Mipango Yako Ya Biashara.

Watu wengi wana hofu za kushindwa, hofu za kukataliwa, hofu za kupoteza, hofu ya kufa, hofu ya kuzungumza mbele ya watu na hofu nyingine nyingi.

Sasa leo nakushirikisha njia moja ya kuweza kuondokana na hofu yoyote inayokufanya ushindwe kuchukua hatua kwenye maisha yako.

Ili kuondokana na hofu, ijaze akili yako mawazo chanya muda wote. Usitoe nafasi yoyote ya mawazo hasi kuingia kwenye akili yako. Mawazo hasi ndio yanayokufanya ushindwe kujiamini na hatimaye uhofie kushindwa.

Jaza akili yako na mawazo ya upendo, amani, na maelewano. Fikiria kuhusu malengo na mipango yako, pata picha ya jinsi maisha yako yatakuwa mazuri kama ukiweza kufikia malengo uliyojiwekea. Itumie picha hii kukusukuma zaidi ili usirihusu mawazo hasi kukuingia na kukurudisha nyuma.

Kama ukiweza kufanya hivi, akili yako ya ndani itakuletea mazingira mazuri yatakayokupa wewe ujasiri na kukuwezesha kufikia chochote unachotaka kwenye maisha yako.

SOMA; Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu Cha Megaliving -By Robin Sharma

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba chanzo cha hofu zangu ni mawazo hasi ambayo yametawala akili yangu. Kuanzia sasa nitakuwa najaza mawazo chanya kwenye akili yangu ili niweze kupata ujasiri wa kuweza kuendea kile ninachotaka.

Tukutane kwenye ukurasa wa 109 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment