Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, April 24, 2015

NENO LA LEO; Hakuna Uhaba Wa Fursa, Kuna Uhaba Wa Kitu Hiki…

There is no scarcity of opportunity to make a living at what you love; there's only scarcity of resolve to make it happen. -Wayne Dyer

Hakuna uhaba wa fursa za kutengeneza kipato kwenye kile unachopenda; kuna uhaba wa wewe kuamua kufanya hivyo.

SOMA; Njia Ya Uhakika Ya Kufikia Mafanikio Makubwa.

Kitu chochote ambacho unapenda kufanya, kuna fursa nyingi sana za kuwez akutengeneza kipato. Kama unapenda kupika keki, unaweza kutengeneza keki kwa ajili ya kuuza, unawez akuandika kitabu chenye maelezo ya jinsi ya kutengeneza keki nzuri, unaweza kurekodi video ukionesha hatua kwa hatua utengenezaji wa keki na mengine mengi ambayo mtu mwingine atakuwa tayari kulipia.

Lakini yote hayo yatatokea kama wewe utaamua yawe hivyo. Kama utakaa chini na kufikiri na kufungua macho yako ili uweze kuziona fursa mbalimbali zinazokuzunguka.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Sababu Namba Moja Kwa Nini Hufanikiwi Kwenye Kazi Unayofanya.

KARIBU KWENYE SEMINA YA MAFANIKIO KUPITIA BIASHARA MWAKA 2015.

AMKA CONSULTANTS imekuandalia semina ya mafanikio kwenye biashara mwaka 2015. Katika semina hii utajifunz amambo yote muhimu yatakayokuwezesha kuanza, kukuza na kufikia mafanikio kwenye biashara yako. Semina itaanza tarehe 04/05/2015 na itaendeshwa kwa mwezi mzima kwa njia ya mtandao(yaani email). Mwisho wa kujiunga na semina hii ni tarehe 01/05/2015. Wahi sasa kujiunga ili upate maarifa yatakayokuwezesha kufanikiwa kwenye biashara. Kwa maelezo zaidi na jinsi ya kujiunga bonyeza maandishi haya.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment