Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, April 12, 2015

NENO LA LEO; Usiweke Maanani Unachoambiwa Na Mtu Aliye Kwenye Hali Hizi Tatu.

It's useless to hold a person to anything he says while he's in love, drunk, or running for office. -Shirley MacLaine

Haina maana kumwajibisha mtu kwa chochote anachosema wakati yuko kwenye mapenzi, amelewa au anagombea.

Katika hali hizi tatu, mtu anaweza kusema jambo lolote hata kama hana uywezo wa kulitekeleza

Mtu aliyepo kwenye penzi zito anaweza kuahidi mambo mengi sana lakini baadae akashindwa kuyatekeleza. Huenda hakuwa anamaanisha ila msukumo wa penzi ulimsukuma afanye hivyo.

SOMA; Hizi Ndio Siri 21 Za Mafanikio

Mtu aliyelewa hii iko wazi, ulevi huwafanya watu waseme mambo ambayo hawajayafikiria kwa kina. Ulevi huathiri uwezo wa mtu wa kuchambua mambo.

Mtu anayegombea nafasi yoyote naye anakuwa kwenye hali ya kutamani sana kushinda. Ili aweze kutimiza hilo yupo tayari kuahidi chochote ili iwe hivyo. Angalia wanasiasa wetu ni vitu vingpi wamekuwa wanaahidi wakati wa uchaguzi na ni vingapi wanatekeleza.

Kwa kujua kwamba mtu yeyote katika makundi haya matatu anaweza kusema jambo ambalo hamaanishi itafanya maisha yako kuwa rahisi kwa kutokuweka matagemeo makubwa kwa watu hawa.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Mafanikio Ya Biashara Yanaanza Na Wewe Mwenyewe.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment