Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, April 22, 2015

NENO LA LEO; Najua Umeshasikia Hili Mara Nyingi, Sio Vibaya Ukasikia Tena Na Leo.

I know you've heard it a thousand times before. But it's true - hard work pays off. If you want to be good, you have to practice, practice, practice. If you don't love something, then don't do it. -Ray Bradbury

Najua umeshasikia hili mara elfu moja kabla. Lakini ni kweli- kufanya kazi kwa juhudi kunalipa. Kama unataka kuwa vizuri, unahitaji KUFANYA, KUFANYA, KUFANYA. Kama kuna kitu ambacho hukipendi, usikifanye.

SOMA; Kazi Ndio Msingi Wa Maendeleo.

Hakuna mbadala wa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa. Nafikiri huwa nasema hili karibu kila siku. Ndio moja ya misingi ambayo naisimamia kwenye maisha yangu. Misingi mingine ni UAMINIFU, UADILIFU na NIDHAMU.

Umeajiriwa, tekeleza majukumu yako kwa ufanisi wa hali ya juu sana. Weka juhudi zako zote na ubunifu wako kuifanya kazi yako kuw aya kipekee, usiangalie ni kiasi gani unalipwa, toa kile ulichonacho wewe kwanza na kama aliyekuajiri hataona thamani yako, wengine wataiona.

Umejiajiri au unafanyabiashara, thamani unayozalisha ndio itakufanya uendelee kuwa na kipato. Weka juhudi na maarifa kwenye kile unachofanya, hakikisha wanatumia bidhaa au huduma zako wananufaika sana.

Kuna kitu ambacho hupendi? Achana nacho, usikifanye, usikifuatilie. Tuna ishi kwneye dunia yenye uhuru mkubwa, hakuna anayekulazimisha chochote, halafu muda ni mfupi sana, mpaka uanze kufuatilia kila kitu.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Njia Mbili Za Kukuondolea Matatizo Yako Ya Kifedha.

KARIBU KWENYE SEMINA YA MAFANIKIO KUPITIA BIASHARA MWAKA 2015.

AMKA CONSULTANTS imekuandalia semina ya mafanikio kwenye biashara mwaka 2015. Katika semina hii utajifunz amambo yote muhimu yatakayokuwezesha kuanza, kukuza na kufikia mafanikio kwenye biashara yako. Semina itaanza tarehe 04/05/2015 na itaendeshwa kwa mwezi mzima kwa njia ya mtandao(yaani email). Mwisho wa kujiunga na semina hii ni tarehe 01/05/2015. Wahi sasa kujiunga ili upate maarifa yatakayokuwezesha kufanikiwa kwenye biashara. Kwa maelezo zaidi na jinsi ya kujiunga bonyeza maandishi haya.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment