Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, April 27, 2015

UKURASA WA 117; Huyu Ndiye Mtu Ambaye Umasikini Huwezi Kumbugudhi.

Umasikini unapenda sana kuwabugudhi watu, lakini sio watu wote. Kuna watu ambao umasikini hupenda sana kuwasumbua. Watu hawa huteseka kwa kipindi kirefu wkenye maisha yao mpaka pale yanapokwisha.

Watu hawa wanaishi maisha yao yote wakitamani kwmaba umasikini uondokane nao lakini jambo hilo linashindikana. Watu hao wanaamini kwamba wakipata fedha tu, basi umasikini bai bai. Ni mpaka pale wanapopata fedha na kugundua kwamba bado umasikini unapenda kuwabugudhi.

SOMA; Siri Hii Itakusaidia Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Wa Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi - 2

Katika hali hii watu hawa huamini kwamba wao walizaliwa ili wawe masikini. Wnakubali kwmaba sio watu wote walizaliwa wawe matajiri na wanatumia kauli nzuri sana kwamba HATUWEZI WOTE KUWA MATAJIRI. Kama kauli hii ni kweli wanashindwa kujiuliza kwa nini wao tu ndio wanaandamwa na umasikini?

Sasa leo nakushiriksiha mtu mmoja ambaye umasikini hauwezi kumsumbua. Mtu huyu umasikini unamuogopa sana na wala hauwezi kumsogelea kwa karibu. Mtu huyu anasifa ambazo hata wewe unaweza kuwa nazo na umasikini ukakuogopa sana.

SOMA; Mambo Muhimu Ya Kuzingati Ili Kupata Mbegu Bora Kwenye Kilimo.

Mtu huyu ana sifa moja kuu, anaamua kuifanya kazi yake kw aubora wa hali ya juu sana kwa sababu anaipenda na anaweka ubunifu ili kuwa tofauti. Huyu ni mtu ambaye anatoa huduma bora sana kupitia kile anachofanya na kila anayekutana naye anafurahia kazi yake. Mtu huyu anaogopewa sana na umasikini kwan sababu hakuna wakati ambao anakosa kazi nzuri ya kufanya. Na kwa kuw aadui wa umasikini ni kazi, mtu huyu ameumaliza kabisa umasikini wka kupenda kazi yake na kuifanya kwa ubora wa hali ya juu sana.

SOMA; BIASHARA LEO; PANGA MARA KUMI.

Je wewe unashidnw akuw ana sifa alizonazo mtu huyu? Najua unaweza, hebu anza sasa. Penda sana kazi unayofanya na ifanye kwa ubora wa hali ya juu sana.

TAMKO LA LEO;

Najua mimi naweza kuw amtu ambaye umasikini unaniogopa sana. Na njia rahisi ya kufanya hivyo ni kupenda sana kazi ambayo ninaifanya na kuifanya kw aubora wa hali ya juu sana kuliko ambavyo imekuwa ikifanywa na wengine. Nitakuwa mbunifu na kuhakikisha kila anayekutana na kazi yangu inamsaidia sana na anaendelea kuwa mteja wangu mzuri.

Tukutane kwenye ukurasa wa 118 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment