Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, April 19, 2015

NENO LA LEO; Hii Ndio Sifa Muhimu Ya Mtu Unayetakiwa Kumuajiri.

Do not hire a man who does your work for money, but him who does it for love of it. -Henry David Thoreau

Usimuajiri mtu anayefanya kazi yako kwa sababu tu anataka fedha, bali ajiri yule anayeifanya kwa sababu anaipenda.

Fedha sio hamasa nzuri ya kufanya kazi. Hii ni kwa sababu hakuna kiwango cha fedha ambacho mtu anaweza kuridhika nacho. Na mtu anapofanya kazi kwa ajili ya fedha tu, hakuna kitu kingine anachojali.

Ila mtu anayefanya kazi wka sababu anaipenda, ataweka juhudi na maarifa, atakuwa mbunifu na hii itamwezesha kufanya kazi yake kwa ubora wa hali ya juu sana. Katika hali hii atakufanyia kazi bora na yeye atapata kipato kizuri.

Nakutakia siku njema.

SOMA; KITABU; Jinsi Ya Kufaidika Na Mabadiliko Yanayotokea Kwenye Maisha.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment