Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, April 15, 2015

NENO LA LEO; Jambo Muhimu La Kufanya Kila Siku Unapoamka Asubuhi.

When you arise in the morning, think of what a precious privilege it is to be alive - to breathe, to think, to enjoy, to love. -Marcus Aurelius

Unapoamka asubuhi, fikiria ni jinsi gani ulivyo na bahati ya kipekee kuwa hai – kupumua, kufikiri, kufurahia, kupenda.

SOMA; TABIA ZA MAFANIKIO; Umuhimu Na Jinsi Ya Kujijengea Tabia Ya Shukrani.

Kama huwezi kufurahia maisha yako kwa vile tu yalivyo unaweza kuwa na maisha magumu sana na maisha yako yatakwenda hivyo kwa muda mrefu.

Shukuru kwa maisha uliyonayo, kuwa hai ni zawadi ya kipekee kwako. Shukuru kwamba unaweza kupumua, shukuru kwamba unaweza kufikiri, shukuru kwamba umeweza kusoma hapa, shukuru kwamba unapenda na kuna wanaokupenda.

Usianze siku yako kwa kufikiria umekosa nini, kwa kufanya hivyo unakosa shukrani. Anza kwa kushukuru kwa vile ambavyo unavyo, ambavyo ni upendeleo mkubwa kwako.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment