Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, April 25, 2015

UKURASA WA 115; Hivi Ndivyo Unavyojitengenezea Dharura.

Maisha sio dharura, ila sisi wenyewe huwa tunayafanya yawe dharura. Kama utakuwa na malengo na mipango yako, halafu ukaifanyia akzi kwa wakati, hakuna wakati wowote ambao utaona una dharura.

Ila hutakuwa na mipango na kufanya mambo pale unapojisikia, kuna wakati utajikuta kwneye dharura kubwa sana. Na hapa ndipo matatizo yote yanapoanzia, pale ambapo una mambo mengi ya kufanya lakini muda ulionao ni kidogo sana.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyodhulumu Maisha Yako Wewe Mwenyewe.

Tunaishi kwenye dunia ambayo ina vitu vingi vya kufanya ila muda tulionao ni ule ule. Una smartphone ambayo inamitandao yote ya kijamii, unaweza kupata habari masaa 24 kwa siku. Hata unapolala, ukiamka tu, habari zipo pale zinakusubiri, uanze kuziperuzi.

Kwa utamu wa habari na kufuatilia mambo mengine kwenye mitandao, inakuwa rahisi kwako kuahurisha yale mambo ambayo ni muhimu sana kwako. Na hapa ndipo unapotengeneza dharura kubwa ambayo itakusumbua sana baadae.

Acha kutengeneza dharura, maisha ni mazuri kama utafanya yale ambayo ni muhimu kwa wakati ambapo umepanga kuyafanya. Mengine yote ambayo sio muhimu achana nayo, hayaongezi chochote kwenye maisha yako na yanakuzuia wewe kufikia mafanikio.

SOMA; Mambo Muhimu Ya Kuzingati Ili Kupata Mbegu Bora Kwenye Kilimo.

TAMKO LA LEO;

Najua kwamba maisha sio dharura japo nimekuwa najitengenezea dharura mimi mwenyewe. Najua dharura sio nzuri kwenye maisha na zitanipelekea kushindwa kufikia mafanikio. Kuanzia sasa nitaacha kufanya mambo ambayo sio muhimu wkangu ili niepuke kujitengenezea dharura.

Tukutane kwenye ukurasa wa 116 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

 

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment