Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, April 16, 2015

NENO LA LEO; Usilenge Mafanikio. Lenga Kitu Hiki Na Mafanikio Yatakuja Yenyewe.

Don't aim for success if you want it; just do what you love and believe in, and it will come naturally. -David Frost

Usilenge mafanikio kama unayataka, wewe fanya kile ambacho unapenda kufanya na amini kwenye kitu hiko na mafanikio yatakuja yenyewe.

Siku zote mafanikio yanakuja kw akufanya kitu ambacho unakipenda. Iwe ni kazi au biashara, hatua ya kwanza ya kufanikiwa ni kukipenda kile unachofanya.

SOMA; Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu Cha Megaliving -By Robin Sharma

Unapopenda unachofanya, unakuwa tayari kujitoa kwa moyo wako wote na unakuwa tayari kuweka juhudi, maarifa na ubunifu ili kutoa kilicho bora zaidi.

Unapotoa kilicho bora ndio unatengeneza njia ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa.

Vipi kama hupendi unachofanya?

Unaweza kufanya mambo mawili.

1. Kipende.

2. Achana nacho na utafute kile unachopenda kufanya.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Siri Za Kuwa Mjasiriamali Bora Na Kufikia Mafanikio Makubwa.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment