Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, April 29, 2015

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutengeneza Biashara Kubwa Kwa Kuanzia Chini Kabisa, Hata Kama Huna Kitu.

Semina ya mafanikio kupitia biashara mwaka 2015 imebaki siku mbili tu ili uweze kujiunga. Kama unapitia changamoto zozote kwenye biashara yako au hata kama huna changamoto ila ungependa kufikia mafanikio makubwa usikose kujiunga na semina hii. Mwisho wa kujiunga ni ijumaa hii tarehe 01/05/2015. Baada ya hapo hutapata tena nafasi ya kujiunga na mafunzo hayo ambayo ni muhimu sana kwenye maisha yako na biashara yako pia. Kujiunga tume fedha ya ada ambayo ni tsh elfu 30 kwenye namba 0717396253/0755953887 na kisha tuma ujumbe wenye jina lako na email yako. Semina itafanyika kwa mwezi mzima wa tano na kwa njia ya email. Kuna vitu unaweza kuvikosa kwenye maisha yako, ila sio semina hii, utakosa mengi na utaendelea kushindwa kufika hatua ya juu kabisa kwenye biashara yoyote ambayo unafanya au unatarajia kufanya.

Kwenye makala ya leo nataka nikushirikishe mbinu ambazo unaweza kutumia na kutengeneza biashara kubwa sana na yenye mafanikio hata kama unaanzia chini kabisa, yaani huna kitu chochote cha kuanzia.

Katika hali ya kawaida watu wengi sana huwa wanalalamika kwamba wanataka kufanya biashara ila hawana mtaji. Wengine wanafikiri wanakosa elimu kubwa ndio maana hawawezi kuingia kwenye biashara. Wengine wanafikiri wangepata ‘connection’ nzuri tu basi biashara zao zingefika mbali sana. Ni kweli vitu vyote hivyo ambavyo watu huwa wanavilalamikia ni muhimu sana ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara. Ila ukweli muhimu zaidi ni kwamba, haimaanishi kwa kukosa vitu hivyo basi wewe umelaaniwa na huwezi kufanikiwa kwenye biashara.

Unaweza kufikia mafanikio makubwa sana kwenye biashara yako hata kama huna mtaji, huna elimu kubwa na hata kama hakuna anayekujua. Inawezekanaje hivyo? Tutajifunza kwa undani sana kwenye semina inayokwenda kuanza wiki ijayo, ila leo hapa nitakuonesha kwa mfano rahisi jinsi gani unaweza kufanya hivyo. Twende pamoja kwenye mfano huu rahisi na unaweza kuutumia kwenye biashara nyingine yoyote.

Tuseme labda wewe ni kijana ambaye umekuwa na wakati mgumu sana kifedha. Unajaribu kutafuta kazi hupati na pia umefikiria sana kufanya biashara ila tatizo limekuwa mtaji. Na pia ukifikiria hakuna mtu yeyote anayeweza kukuunganisha na watu wa kazi au watu wa biashara. Ukifikiria mkopo, hupati jibu kabisa kwa sababu huna chochote cha kuweka dhamana.

Ila kwa kuwa wewe ni mtu ambaye hukatishwi tamaa haraka, unaamua kufikiria zaidi. Unajiuliza ni shida gani ambayo mtu anaweza kuwa nayo na wewe ukaweza kuitatua na akakupa japo fedha kidogo? Kwa kufikiria kwa kina na kutokana na hali uliyonayo, unapata jibu moja ambalo linakuonesha mwanga. Unagundua kwamba sehemu unayoishi watu wana magari, ila hawapati huduma nzuri za kuoshewa magari yao. Unaona hapa ndio unapoweza kuanzia, kuosha magari kwa mtindo tofauti kabisa na wanavyofanya wengine.(Tafadhali usiishie hapa baada ya kuona nakuambia ukaoshe magari, hii ni hatua ya mwanzo tu, utafikia biashara kubwa sana baadae). Baada ya kuwa na wazo hili unaweza kulikuza hatua kwa hatua kama ifuatavyo.

Nenda kwa kila jirani mwenye gari, na mweleze kwamba ungeomba umwoshee gari yake bure kabisa. Unamwambia unataka kuanzisha biashara ya kuosha magari ambayo itakuwa tofauti kabisa na inavyofanyika sasa. Mwambie kwamba kwa ufahari wa huduma hii anafanyiwa akiwa nyumbani kwake, kwa siku ambayo amepumzika. Utahitaji kutoa maelezo ya kina ili uonekane kwmaba unajua kile ambacho unakwend akufanya. Kuna ambao watakataa, ila wengi watakubali, kwa sababu hakuna gharama yoyote wanayoingia na kama umewapa maelezo mazuri, watajaribu kupima waone kama kweli huduma unayokwend akuwapa ni ya tofauti.

Baada ya hapo jifunze kila aina ya gari unaloona majirani zako wanalo. Kama umeweza kusoma hapa, maana yake unawez akufungua mitandao mbalimbali inayohusiana na magari. Jifunze ubora wa gari husika, tafuta kitu chochote unachoweza kukisifia kwenye gari la mteja wako. Jua vitu muhimu unavyoweza kumshauri kuhusiana na gari lake hilo ili liweze kudumu kwa muda na lisimsumbue. Wakati huo huo jifunze kuhusu uoshaji wa magari, Jifunze ni kemikali gani nzuri unazoweza kuzitumia na zisilete madhara kwenye rangi ya gari au vitu vingine kwenye gari. Mambo yote haya muhimu utamweleza mteja wako siku ya kwanza unapoomba kuosha gari bure na hata siku ya kufanya kazi hiyo. Pia waeleze ni jinsi gani itakuwa fahari kwao kw akupata mtu wa kuwaoshea magari huku akiwapatia maelekezo yote ya msingi kuhusiana na magari yao.

Baada ya kupata nafasi ya kuosha gari bure kwa siku ya kwanza, hapa sasa unatoa ofa yako ambayo mteja hawezi kuikataa kutokana na huduma nzuri uliyompatia siku hiyo ya kwanza. Mwambie mteja kwamba unaweza kumfanyia huduma hiyo mara moja kila wiki kwa gharama ya tsh elfu tano tu. Utamfanyia usafi wa uhakika na kumpa maelekezo yote muhimu kuhusiana na gari lake.

Labda tuseme kwenye mtaa unaokaa kuna watu 30 ambao wanamiliki magari yao. Kwa kuongea nao wote 20 wanaweza kukubali kukupa nafasi ya kuwaoshea magari yao bure. Baada ya kutoa huduma hii ya kwanz a bure na kuwapa ofa yako, tuseme 10 ndio watakaosema ndio. Hii ni sawa na tsh elfu 50 kwa wiki, kwa kuanzia, sio mbaya ukilinganisha na sasa ambapo huna kipato kabisa. Na kumbuka huu ni mwanzo tu, unaendelea kuwaambia wengine wengi zaidi, maliza mtaa unaokaa na nenda mtaa mwingine. Na hawa wateja wako waambie wawaambie na marafiki zao kwamba unatoa huduma hiyo. Uzuri ni kwmaba mtu mwenye gari atakuwa na marafiki ambao nao pia wana magari na kama ukiwapa huduma nzuri hawatasita kuwaambia wenzao kwamba kuna kijana anatoa huduma nzuri sana ya kusafisha magari.

Hata kama umepata mteja mmoja, endelea kuongea na wengine wengi. Hata kama wote wamekataa, endele akuongea na wengine wengi, na kama utakuwa unatoa maelezo yako vizuri kuna mtu atakuambia NDIO na huyu ndio wa kumtumia vizuri.

Kumbuka katika mchakato wote huu hujatumia fedha nyingi sana, hujahitaji kuw ana eneo kwa sababu huduma hii unaitolea kwa mteja. Labda utahitaji kuwa na ndoo mbili, na vifaa vingine vya kawaida vya kuoshea na sabuni au kemikali nyingine nzuri ya kuoshea magari ambayo sio ya bei ghali sana. Gharama za vitu hivyo vichache haiwezi kuzidi tsh elfu 20.

Haya yote tuliyojadili hapo juu ni hatua ya kwanza kabisa ya wewe kufanikiwa kwenye biashara, bado kuna hatua nyingi sana ambazo bado hujatumia. Na changamoto kubwa ni kwmaba watu wengi huwa wanaishia hatua hii ya kwanza ndio maana wanakuwa watumwa wa biashara zao. Unakuta mtu anauza duka lile lile kwa kiwango kile kile kwa zaidi ya miaka 10, hakuna mafanikio hapa. Sasa wewe hutaki kuosha magari kwa maisha yako yote. Hivyo unakwenda hatua nyingine muhimu kabisa ya ukuaji wa biashara yako. Anza kutoa huduma za ziada kwenye magari unayoosha, badilisha oil au maji au chochote ambacho kutakuongezea kipato cha ziada kutoka kwa mteja wako ambaye sasa anakuamini sana. Unaweza pia kuchukua jukumu la kuwatafutia fundi wa uhakika kwa matatizo wanayokutana nayo kwenye magari yao. Yaani wewe unakuwa zaidi ya muosha magari kwao, wanapopata shida yoyote kwenye magari yao, mtu wa kwanza kuja kwenye akili yao ni wewe na hivyo kukutafuta uwashauri vizuri.

Baada ya kupata wateja wa uhakika tafuta vijana wengine ambao wapo tu mtaani na hawana cha kufanya. Chagua unaoona wanaweza kufanya akzi kwa uaminifu, wafundishe kile unachofanya na wafenye kuwa wasaidizi wako. Walipe kadiri wanavyoweka juhudi zao kwenye kazi unazowapangia. Endelea kwenda mbele, endelea kukua, endelea kuongeza wateja mpaka unafikia wateja 1000 kwa mwezi ambao wapo tayari kukupa sio chini ya shilingi elfu tano kila mmoja. Hii itakuwa ni milioni tano, ukiondoa gharama zote za uendeshaji, bado utabaki na zaidi ya nusu ya kiwango hiko. Sasa niambie ni nani angekuajiri akupe mshahara wa milioni mbili, ndani ya mwaka wako wa kwanza wa kazi. Kumbuka hapa bado una nafasi kubwa ya kuendelea kukua zaidi na zaidi na hakuna kikomo isipokuwa unachojiwekea mwenyewe.

Hivyo ndio unavyoweza kutengeneza biashara kubwa kw akuanzia chini kabisa. Maelezo hayo yanaonekana rahisi ila utekelezaji unahitaji moyo, unahitaji muda maana hiyo haitotoke amara moja tu, watu watataka wakuamini kwanza ndio waweze kufanya kazi na wewe. Unahitaji uaminifu wa hali ya juu sana, unahitaji kujitoa na kutokujali wengine wanakuchukuliaje kwa sababu umeamua kuosha magari. Unahitaji uvumilivu, kuna watu watakuambia hapana, kuna wengine watakusumbua kwenye malipo. Lakini kama utakomaa, kama utaweka juhudi na maarifa na ukatoa huduma ambayo mtu hajawahi kuipata kokote, lazima utakuwa na bishara, hata kama hutofikia mamilioni, lakini utapata cha kukutoa hapo ulipo.

Sasa hebu niambie, unafikiri ni kitu gani kinachokuzuia mpaka sasa? Ni wewe mwenyewe tu.

Mfano huu tuliotumia hapo juu unawez akuweka kitu kingine chochote unachoweza kufanya, iwe ni kutangaza biashara za watu wengine kwenye mtandao, iwe ni kutoa huduma ya kukusanya taka taka, iwe ni kutoa huduma ya kufundisha watoto majumbani na mengine mengi. Unachohitaji ni wewe kukaa chini, kuweka mipango na kuanz akuitekeleza mara moja.

Kupitia semina inayoanza wiki ijayo, utajifunza mengi zaidi na jinsi unavyoweza kubadili wazo lolote kuwa biashara itakayokulipa.

Kama wewe ni kijana na huna fedha kabisa ila umependezwa na wazo hilo hapo juu na unafikiria kulifanya, jiunge na semina hii halafu tutapata muda wa kuendeleza wazo hilo na nitakupa nafasi ya kuwa msimamizi wako mpaka biashara yako itakapokomaa. Kwa hiyo unahitaji shilingi elfu 50, elfu 30 ya semina na elfu 20 ya kuanzia biashara yako. Kama kwa kufikiria wkako kote unaona huwezi kupata shilingi elfu 50, fanya hivi, angalia ni vitu gani unavyomiliki ambavyo huna matumizi navyo makubwa na unaweza kuuza na kupata fedha hiyo. Kama huna, angalia katika ndugu zako na watu wengine wa karibu, chagua watu kumi ambao utaomba kuonana nao na utawaomba wakupe shilingi elfu kumi tu kila mmoja, waambie kuna kitu cha tofauti unataka kujaribu na kitakuw ana manufaa kwako. Katika 10 utakaowaomba, hutakosa watano watakao kupatia. Usikubali kirahisi, pambana mpaka uhakikishe umepata kile ambacho unakitaka.

Nikukaribishe sana kwenye semina inayoanza wiki ijayo na mwisho wa kujiunga ni ijumaa hii. Ukiikosa hii, unakuw aumejikosesha mambo mengi sana na mazuri.

Nakutakia kila la kheri katika biashara unayofanya au unayotegemea kufanya.

TUPO PAMOJA

Makirita Amani 

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

kitabu-kava-tangazo4322

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment