Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, April 5, 2015

Salamu Za Sikukuu Kutoka AMKA CONSULTANTS Na Mambo Muhimu Kwako Kuzingatia.

Leo ni sikukuu ya pasaka ambapo wakristo wote duniani wanaadhimisha mateso na kufufuka kwa mwokozi wao Yesu Kristo. Vile vile leo ni siku ya mapumziko kwa Watanzania wote.

Kampuni ya AMKA CONSULTANTS ambayo ndio inasimamia mitandao hii AMKA MTANZANIA, KISIMA CHA MAARIFA, MAKIRITA AMANI NA JIONGEZE UFAHAMU inachukua nafasi hii kukutakia wewe mtanzania sikukuu njema na mapumziko mema pia.

Katika sikukuu hii umekuwa na siku nyingi za mapumziko na kusherekea pia. Sherekea sikukuu hizi kwa amani na upendo na kumbuka kwamba kuna maisha baada ya sikukuu hizi.

Pia katika muda huu mrefu wa mapumziko, kumbuka kupata muda wa kufanya jambo ambalo ni muhimu kwako na ambalo hukupata muda wa kulifanya katika siku za kawaida.

AMKA CONSULTANTS itaendelea kuwa nawe katika safari ya kuboresha maisha yako. Lengo letu ni kufanya kazi na watu ambao wapo tayari kuchukua hatua ya kuboresha maisha yao na kuwasaidia kufikia lengo lao hilo. AMKA CONSULTANTS tunajua kwamba unawez akubadili maisha yako kama utakuwa tayari na kama ukipata msaada wetu ambao ni muhimu sana kwako.

Tutaendele akuwa nawe katika kila hatua ya maisha yako, kazi yako na hata biashara yako.

Endelea kutembelea mitandao yetu kila siku ili kujifunza, kuhamasika na kushauriwa. Tunakuahidi kupata huduma bora sana kulingana na mahitaji yako.

Karibu sana tufanye kazi pamoja.

Nawatakia watanzania wote sikukuu njema na mapumziko mema.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Mkurugenzi, AMKA CONSULTANTS.

N;B Kwa ushauri zaidi wa kibiashara, ikiwepo jinsi ya kupata wazo bora la biashara, jinsi ya kuanza na kukuza biashara na jinsi ya kupambana na changamoto za biashara piga simu 0717396253.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment