Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, March 28, 2015

Njia Moja Ya Uhakika Ya Kuishinda Hofu.

Ili kuishinda hofu, rudisha mawazo yako kwenye wakati uliopo sasa. Maana hofu kubwa unaipata pale unapofikiri mambo yaliyopita ambayo huwezi kuyabadili na kuwaza mambo yajayo ambayo huwezi kuyabadili pia.
Acha kuwaza mambo ambayo yameshapita, huwezi kuyabadili. Yatakuumiza na kukupa hofu kubwa.
Acha kufikiria mambo yajayo na kuyahofia. Bado hujayafikia na mambo hayatakuwa mabaya kama unavyofikiria sasa.
Weka mawazo yako sasa, kwenye wakati uliopo na utapata ujasiri mkubwa wa kufanya kile unachotaka kufanya.
Kumbuka ili kuwa na maisha mazuri ya kesho unatakiwa kuwa na maisha mazuri leo. Hivyo badala ya kuhofia kesho itakuwaje, tumia muda huo kuishi vizuri leo na kesho mambo yatakwenda vizuri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment