Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, March 29, 2015

NENO LA LEO; Kama Tayari Una Ndoto Hiki Ndio Unatakiwa Kufanya.

“If you have a dream, don’t just sit there. Gather courage to believe that you can succeed and leave no stone unturned to make it a reality.” ― Roopleen

Kama una ndoto, usikae tu na kufikiri utaifikia. Kusanya ujasiri wa kuamini kwamba unaweza kufanikiwa na usiache jiwe lolote halijageuzwa kwenye kutimiza ndoto zako.

Karibu kila mmoja wetu ana ndoto kubwa sana kwenye maisha yake. Ila watu wengi hukaa na ndoto zao bila ya kufanya jitihada zozote kubwa za kutimiza ndoto hiyo.

SOMA; Nilichojifunza Leo; Zoezi Moja Litakalobadili Maisha Yako Kabisa.

Mtu anaweza kukuambia nina ndoto za kuwa mfanyabiashara mkubwa. Ukimuuliza umeshafanya nini ili kufikia ndoto hiyo anaanza kukuletea sababu. Mara mtaji sina, mara sijapata wazo na mengine mengi. Kama kweli ndoto yako ni kuwa mfanyabiashara mkubwa, unatakiwa kuanza kuhangaika huko na kule, kuhakikisha unapata pa kuanzia. Unaongea na watu wengi, unajaribu vitu vingi mpaka unapata kitu kimoja cha kukomaa nacho.

Nakutakia siku njema.

SOMA; BIASHARA LEO; Biashara Unayofanya Sasa, Au Utakayoanza Sasa Sio Biashara Utakayofanya Milele.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment