Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, March 31, 2015

NENO LA LEO; Kitu Kimoja Unachohitaji Kuondoa Ili Kufanikiwa.

“You crave winning and fear losing instead of just doing. To succeed you must remove your self-imposed limitations.” ― Wayne Gerard Trotman

Unatamani kufanikiwa na unahofia kushindwa badala ya kufanya. Ili kufanikiwa unahitaji kuondoa vikwazo ulivyojiwekea mwenyewe.

Hakuna ambaye hatamani kufanikiwa, lakini kutamani tu hakutakuletea mafanikio unayotazamia.

Watu wengi sana wana hofu ya kushindwa. Wanaogopa kufanya jambo kwa sababu wanafikiria kama watashindwa hali itakuwaje? Wanaona kama watapoteza au maisha kuwa magumu zaidi.

SOMA; BIASHARA LEO; Mwisho Wa Ufalme Wa Mteja.

Hapo ulipo kuna vikwazo vingi sana ambavyo umejiwekea mwenyewe. Kumbuka yale maneno unayojiambia kwamba huwezi kufanya biashara kwa sababu huna mtaji, huwezi kufikia uhuru wa kifedha kwa sababu huna elimu kubwa. Na mengine mengi, yote haya yanakurudisha nyuma.

Mafanikio yanatokana na kufanya, yanatokana na vitendo.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Tabia Hizi Zitakusaidia Sana Kufikia Malengo Yako Kwa Haraka.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment