Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, March 19, 2015

NENO LA LEO; Haya Ndio Maafa Unayojitengenezea Mwenyewe.

“As long as you look for someone else to validate who you are by seeking their approval, you are setting yourself up for disaster. You have to be whole and complete in yourself. No one can give you that. You have to know who you are - what others say is irrelevant.” ― Nic Sheff

Kama bado unasubiri wengine wakukubali vile ulivyo kwa kufanya wanachotaka wao, umejiandalia maafa. Unahitaji kuwa vile ulivyo wewe mwenyewe, hakuna anayeweza kukupa hilo. Unatakuwa kujua wewe ni nani, wanayosema mengine hayana maana.

SOMA; Jinsi ya kuchagua Kampuni ya kuwekeza katika Soko la Hisa

Wewe ni wewe, hakuna mwingine kama wewe dunia nzima.

Usikubali kuiga kile wengine wanachofanya ili tu wakukubali, kuwa ulivyo wewe na kama wanakujali watakukubali vile ulivyo na watakuheshimu sana.

Ila ukianza kutengeneza maisha tofauti ili tu watu wakukubali, hawatakukubali na watakudharau kabisa. Hii ni kwa sababu hakuna mtu anayependa mtu ambaye sio halisi.

Kuwa halisi, kuwa wewe, jiamini, jikubali. Fanya kile unachofanya vizuri, wanaokujali watakuwa pamoja na wewe, wasiokujali, hata ungefanya nini bado usingeweza kuwashawishi.

Nakutakia siku njema.

SOMA; Jinsi Ya Kuondokana Na Hofu Ya Kuongea Mbele Za Watu.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment