Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, September 23, 2014

Watu Watatu(3) Waliofukuzwa Kwenye Kampuni Walizoanzisha Wenyewe.

Unaweza kufikiri kuingia kwenye biashara na kujiajiri mwenyewe ndio njia nzuri ya wewe kuwa na uhuru kwa kile unachofanya. Inaweza isiwe kweli kwa sababu kwa jinsi hali ya biashara za kisasa ilivyo unaweza kujikuta kwenye hali ngumu sana.

Tena pale unapofikia kampuni ikawa kubwa na kuanza kuuza hisa, wenye hisa nyingi wanaweza kufanya maamuzi hata ya kukufukuza wewe japo wewe ndiye uliyeanzisha.

Hapa ni orodha ya watu watatu ambao walifukuzwa kwenye kampuni walizoanzisha wenyewe;

1. Steve Jobs, Apple

Steve Jobs alianzisha kampuni ya apple ila baadae alifukuzwa kwenye kampuni hiyo. Alikuja kurudishwa kwenye kampuni hiyo na kuleta mapinduzi makubwa ya kiteknolojia.

2. Ted Tunner, CNN

Ted Tunner alianzisha CNN, shirika la habari la marekani lakini baadae alikuja kufukuzwa kwenye shirika hilo.

3. Jack Dorsey, Twitter

Jack Dorsey ni mmoja wa waanzilishi wa mtandao wa kijamii unaoitwa twitter ila kwa sasa anaonekana hayupo tena kwenye mtandao huo kwani ameanzisha kampuni nyingine ya teknolojia.

Kuwa makini pale unapoanzisha kampuni yako yasije kukutokea mambo ambayo hukutarajia.

Nakutakia kila la kheri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment