Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, September 20, 2014

Hivi Ndivyo Mitandao Ya Kijamii Inavyoharibu Akili Yako, Kuwa Makini.

Tunaweza kukubali kwamba mitandao ya kijamii ndio mapinduzi ya sasa. Yaani kama ilivyokuwa mapinduzi ya viwanda, sasa tuna mapinduzi ya mitandao ya kijamii. Mitandao kama facebook, twitter, instagram, linked in na mingine mengi imekuwa sehemu ya maisha yetu.

Mitandao hii imekuwa na faida kubwa sana, kuwaleta watu karibu zaidi ya ilivyowahi kutokea. Watu wengi wamefahamiana kupitia mitandao hii na wengine wanatengeneza kipato kupitia mitandao hii.

Kama tunavyojua, chochote chenye faida huwa kina hasara. Leo tutaangalia hasara ya mitandao ya kijamii kwenye akili yako na hivyo kuharibu maisha yako.

Kwenye mitandao hii ya kijamii kwa mfano facebook au instagram, watu huweka picha zao mbalimbali wakiwa katika hali ya furaha au kustarehe. Kupitia picha hizi kama na wewe hujapata nafasi ya kuwa katika hali hizo unaweza kuona maisha yako sio mazuri kama ya wale ambao wanaweka picha nzuri.

Kwa mfano mtu anaweka picha anakula vyakula vizuri anakuandikia I AM HAVING LUNCH, wakati huo wewe unakula makande au wali maharage ni manyanyaso makubwa sana kisaikolojia. Hali kama hii inakufanya wewe ujione maisha yako sio mazuri kama ya watu hao.

Kitu unachotakiwa kukumbuka ni kwamba watu hawa wameweka picha hizo nzuri chache tu, kuna siku wanakula makande kama wewe ila hawaleti picha zao kwenye mitandao. Kuna siku wanashinda njaa ila hawatakuandikia kwamba wameshinda njaa.

Hivyo acha kujilinganisha na chochote unachokiona kwenye mtandao wa kijamii. Kama mtu kaweka picha anakula vizuri au kavaa vizuri au yuko kwenye kiwanja kizuri usijaribu kujilinganisha hata kidogo. Maisha yako wewe yanaweza kuwa bora kuliko hata ya watu hao.

Tumia mitandao ya kijamii kujumuika na wengine ila isiwe sehemu ya wewe kujilinganisha na wengine na hatimaye kuona maisha yako hayana thamani.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

2 comments:

  1. Ni kweli kabisa ndugu.

    ReplyDelete
  2. Sometimes mitandao ya kujamii inaleta changamoto,unaweza ukajiona bado upo nyuma na ikakufanya uongeze juhudi zaidi.

    ReplyDelete