Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, September 24, 2014

Mambo Matano(5) Ambayo Ni Marufuku Kufanya Kwenye Eneo La Kazi.

Kazi ndio msingi wa maendeleo. Na ili uweze kufikia mafanikio makubwa ni lazima ufanye kazi kwa bidii na maarifa. Sifa moja kubwa ya kufanikiwa kwenye kazi yoyote ni kupenda unachofanya. Kuna mambo mengi sana ambayo ukiyafanya kwenye kazi yako yanakuzuia kufikia mafanikio.

Leo JIONGEZE mambo haya matano ambayo ni marufuku kuyafanya eneo la kazi kama unataka kufikia mafanikio makubwa.

1. Kuonesha tabia ya hasira au kulipiza kisasi.

Mara kwa mara mtapishana kauli na mfanyakazi wako, mfanyakazi mwenzako au bosi wako. Kwa vyovyote vile tafuta njia ya kumaliza tofauti zenu kwa amani, ukiongea au kufanya mambo kwa hasira au kupanga kulipiza kisasi utaingia kwenye matatizo makubwa.

2. Majungu na kusengenya.

Maeneo mengi ya kazi hapa Tanza ia kuna majungu mengi sana. Usianzishe wala usishiriki kumpiga jungu mtu yeyote aliyepo kwenye eneo lako la kazi. Ni kumkosea heshima na hii itakufanya uingie kwenye matatizo.

3. Kudanganya.

Wafanyakazi wengi wamezoea kudanganya hapa na pale. Tatizo kubwa la kudanganya kwenye eneo lako la kazi ni kwamba itakubidi uishi uongo huo kwa muda mrefu kitu ambacho kitakuumiza.

4. Kuchukua sifa za wengine.

Kuna watu wanasubiri wengine wafanye kazi halafu wao ndio wanaokuwa wa kwanza kusema kama sio mimi hiki kisingewezekana. Usifanye hivi, utakosa ushirikiano kutoka kwa wengine. Kila mtu ana nafasi kubwa kwenye kukamilika kwa jambo lolote.

5. Usichome daraja.

Watu wengi wanaojiajiri wanatokea kwenye ajira. Zamani kidogo watu walikuwa wakiondoka kwenye ajira zao kwa ugomvi mkubwa na hivyo kuondoa kabisa ushirikiano. Wewe usifanye hivi, kama unakwenda kujiajiri hakikisha unakuwa na uhusiano mzuri na mwajiri wako kwani anaweza baadae kuwa mteja wako au akakuletea wateja. Mafanikio ya sasa yanatokana na ushirikiano mzuri uliojenga na watu.

Epuka kufanya mambi hayo matano kwenye kazi yako kama kweli unataka kupata mafanikio kupitia kazi hiyo.

Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment