Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, September 24, 2014

Ukiacha Kuangalia Facebook Kila Mara Mambo Haya Matano Yatatokea.

Facebook ni mtandao mkubwa sana wa kijamii ambao unaongoza kwa kuwa na watumiaji wengi. Facebook imekuwezesha kujuana na watu wengi, kukutana na marafiki mliopotezana zamani na hata kujifunza mambo mengi. Hata makala hi unaweza kuwa umeipata kupitia facebok.

Pamoja na faida hizi, facebook imekuwa chanzo kikubwa cha watu wengi kupoteza muda kwani ina utegemezo mkubwa. Unaweza kujikuta kila siku unaangalia ni nini kinaendele kwenye facebook.

Kama utaacha kuangalia facebook kila mara, mambo haya matano yatatokea.

1. Utaacha kufa akili.

Kila mara unapotumia facebook ni kama akili yako inakuwa imekufa. Kwa sababu unajikuta akili yako yote imeingia kwenye mtandao huo na hivyo kushindwa kuona na kufikiria mambo mengine yanayoendelea. Kwa mfano unaweza kuwa umepanda gari safari nzima uko kwenye facebook tu na hivyo kushindwa kuona vitu vingine ambavyo vingekufanya ufikiri zaidi.

2. Utakamilisha kazi nyingi.

Kila mara unapoingia facebook hasa kwenye kuda wa kazi ni kama unajiibia muda wako wa kazi. Hivyo ukiweza kujidhibiti na ukapunguza muda unaoingia kwenye mtandao huu utakamilisha kazi nyingi.

3. Utawajua marafiki zako wa kweli ni kina nani.

Kupata marafiki kwenye mtandao ni rahisi sana. Unaweza kulike post zao au kuweka maoni kila mara na tayari mkawa karibu. Ila urafiki wa ukweli unahitaji zaidi ya hapo. Hivyo punguza muda unaotumia kwenye mtandao na ujue marafiki zako wa kweli ni watu gani.

4. Utaacha kujilinganisha na wengine na hivyo kujikubali.

Facebook inaweza kuwa sehemu ya kukufanya uone hakuna unachofanya cha maana. Hii inatokana na kuona wengine wakifanya mambo makubwa. Wakati mwingine unachokiona sio kweli.

SOMA; HIvi ndivyo mitandao ya kijamii inaharibu akili yako, kuwa makini.

5. Utagundua ulikuwa unatumika kibiashara.

Facebook zamani ilikuwa nzuri sana ila kwa sasa hivi wanatumia taarifa zako kuwauzia watu wa matangazo. Hivyo kila utakapoingia utakutana na matangazo na post nyingi za marafiki zako hutaziona tena. Kwa njia hii facebook wanakutumia wewe kibiashara.

Tumia mitandao ya jamii lakini usikubali mitandao hii ikutumie wewe.

Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment