Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, September 16, 2014

Mambo 10 Rahisi Unayoweza Kuanza Kufanya Leo Na Ukaboresha Maisha Yako.

Safari ya maisha ni safari yenye changamoto nyingi sana. Katika safari hii kuna milima na mabonde na hata visiki vinavyoweza kukukwamisha. Ili kuweza kushinda changamoto hizi kuna vitu vidogo vidogo sana unavyoweza kufanya kila siku na ukaboresha maisha yako.

 

Haya hapa ni mambo 10 unayoweza kuanza kufanya leo na ukaboresha maisha yako.

1. Kuwa na mtazamo chanya. Katika kila jambo linalotokea jua kuna kitu kizuri cha kujifunza au kunufaika.

2. Kunywa maji mengi. Sehemu kubwa ya mwili wako ni maji, ukosefu wa maji unaweza kukufanya upate matatizo ya kiafya.

3.  Jenga tabia ya kujisomea. Tabia hii itakufanya uweze kufikiri zaidi na pia utajifunza zaidi. Kama huna kitabu cha kusoma bonyeza hapa na uweke email yako utatumiwa vitabu.

4. Jifunze kusema hapana. Matatizo mengi unayokutana nayo kwenye maisha yako yanatokana na wewe kukubali kila kitu unachokutana nacho au unachoambiwa. Anza leo kusema hapana.

5. Acha kutumia simu yako kwa muda. Simu za kisasa zimetufanya tuwe watumwa wa kila mara kuangalia nini kinaendelea. Anza leo kuzima simu yako japo kwa saa moja na utumie muda huu kufanya mambo mengine.

6. Pata kifungua kinywa. Watu wengi wanakosa kifungua kinywa kwa sababu ya haraka au kupunguza matumizi, usifanye hivi.

7. Usitumie zaidi ya unachopata, hakikisha matumizi yako yanakuwa pungufu ya kipato chako.

8. Acha kulalamika. Kama kuna kitu hukipendi kibadilishe, kama huwezi kukibadilisha achana nacho.

9. Omba msaada. Huwezi kufanya kila mwenyewe, unahitaji msaada wa watu wengi.

10. Kaa mbali na watu wenye kukatisha tamaa. Ukiwa karibu nao watakurudisha nyuma.

Maisha unayoishi ni yako na una uwezo wa kuyabadili na kuyafanya vile unavyotaka wewe. Anza leo kwa kufanya mambo hayo rahisi na utaona mabadiliko makubwa.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment