Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, September 18, 2014

Mambo 10 Unayotakiwa Kuacha Kufanya Ili kuboresha Maisha Yako.

Maisha yetu ya kila siku yana changamoto nyingi sana. Lakini sehemu kubwa ya changamoto hizi tunasababisha wenyewe kutokana na maamuzi tunayofanya au tabia zetu wenyewe.

Hapa kuna mambo kumi ambayo unatakiwa uache kuyafanya ili uweze kuwa na maisha bora.

1. Acha kulalamika sana kwenye maisha yako. Kulalamika hakutakusaida zaidi ya kukufanya ujione huna msaada. Kama kuna kitu hukipendi kibadilishe, kama huwezi kukibadilisha achana nacho.

2. Acha kujiongezea msongo wa mawazo. Usijipe kazi nyingi kupiata uwezo wako, usiahidi mambo mengi na usijaribu kufanya kila kitu.

3. Acha kujutia makosa uliyofanya zamani. Kuendelea kujutia kila siku na kukumbuka ulichopoteza au ulichokosa hakutakusaidia chochote zaidi ya kukuumiza. Jifunze kutokana na makosa hayo na songa mbele.

4. Acha kuhofia kesho yako na anza kufanyia kazi ndoto zako. Hofu ni kitu ambacho hakipo ila kinakuzuia wewe kufikia mafanikio makubwa. Achana na hofu sasa na fanya kitu kufikia ndoto zako.

5. Acha kusogeza mambo mbele na anza leo. Umesema unataka kuanza biashara ila utaanza kesho, kesho haitafika, anza leo kuweka mipango yako na anza kuifanyia kazi.

6. Acha kutegemea watu wengine ndio wakupe furaha, kumbuka furaha inatoka ndani yako.

7. Acha kulinganisha maisha yako na ya watu wengine. Hakuna mtu mwenye uwezo ambao unao wewe. Kazana kuwa bora kila siku ila sio kujilinganisha na wengine.

8. Acha kusubiri muda muafaka. Unasubiri muda muafaka ndio uanze biashara? Muda muafana ndio sasa, hutapata muda mwingine mzuri kama huu kufanya kile ambacho unataka kufanya.

9. Acha kukimbia matatizo yako. Kukimbia matatizo sio kuyasuluhisha, yataendeleakukufata ulipo. Yakabili matatizo yako na uyatatue.

10. Acha kukaa na watu wanaokurudisha nyuma. Watu unaokaa nao wana ushawishi mkubwa sana kwako. Kama unakaa na watu waliokata tamaa na wanaolalamika tu na wewe utakuwa hivyo hivyo.

Boresha maisha yako kwa kuacha kufanya mambo haya ambayo yanakurudisha nyuma.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment