Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, September 29, 2014

Mambo Matano Ya Kushangaza Kuhusu Siku Ya Jumatatu

Jumatatu ni siku ya kwanza ya wiki. Ni siku ambayo watu wanatoka kwenye mapumzimko na kuanza tena wiki ya kazi. Na kwa kuwa watu wengi hawapendi kazi wanazofanya, jumatatu inaonekana kuwa siku mbaya sana.

Haya ni mambo matano ya kushangaza ambayo hutokea sana siku za jumatatu tofauti na siku nyingine za wiki.

1. Zaidi ya asilimia 50 ya wafanyakazi huchelewa kazini.

Tafiti nyingi zinaonesha jumatatu ndio siku ambayo inaongoza kwa watu kuchelewa kufika kazini au kuwa watoro kazini.

SOMA; Mambo matano ya kufanya siku ya jumatatu ili uwe na wiki yenye mafanikio.

2. Asilimia kubwa ya watu hujiua.

Tafiti zilizofanywa hasa kwenye nchi zilizoendelea zinaonesha kwamba jumatatu ndio siku ambayo inaongoza kwa watu kujiua.

3. Asilimia kubwa ya watu hupata shambulio la moyo.

Jumatatu ndio siku ambayo watu wengi hupata shambulio la moyo(heart attack) zaidi ukilinganisha na siku nyingine za wiki. Hii inaweza kusababishwa na shinikizo kubwa la damu kutokana na kurejea kwenye kazi.

4. Mvua hainyeshi sana.

Inasemekana siku za jumatatu haina mvua sana ukilinganisha na siku nyingine za wiki. Hii inatokana na kwamba mwisho wa wiki watu wengi hawafanyi kazi na hivyo hakuna uchafuzi mkubwa.

5. Ni siku nzuri ya kununua gari.

Jumatatu ni siku nzuri ya kununua gari kwani wauzaji wa magari wanakuwa wameuza sana mwishoni mwa wiki na hawategemei wateja wengi siku ya jumatatu hivyo kuwa tayari kupunguza bei kwa kiasi kikubwa.

Nakutakia jumatatu njema na epuka mambo yanayoweza kukuharibia maisha yako hasa yanayotokea siku za jumatatu.

Tuko pamoja.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment