Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, September 19, 2014

Faida Tano (5) Za Kulala(Kusinzia) Mchana.

Katika jamii zetu kulala mchana inaweza kuonekana kama uvivu. Yaani mtu anayelala mchana anaonekana ni mvivu na hapendi kazi. Kinyume na imani hii kulala mchana kuna faida kubwa sana kuliko ulivyowahi kufikiri.

Leo utajifunza faida tano za kulala mchana na kama utaweza uweke ratiba hiyo kwenye kila siku yako.

1. Inapunguza stress.

Kufanya kazi kwa siku nzima inaweza kukufanya uwe na stress nyingi sana. Kupata dakika chache za kulala inapunguza stress hizi.

2. Inaongeza uwezo wa kujifunza na kumbukumbu.

Ni rahisi sana kujifunza na kukumbuka yale uliyojifunza kama akili inakuwa imepumzishwa. Kulala mchana kunaipumzisha akili.

 

3. Inaongeza ubunifu.

Kama unafanya kazi ambazo zinahitaji ubunifu wa hali ya juu kuwa na utaratibu wa kulala mchana na unapoamka unakuwa katika nafasi nzuri ya ubunifu.

4.  Ni bora kwa afya yako.

Tafiti zinaonesha kwamba watu wanaolala mchana wanauwezekano mdogo wa kupata magonjwa ya moyo ukilinganisha na ambao hawalali mchana.

5. Inaongeza ufanisi.

Watu ambao wanalala mchana huamka wakiwa na ufanisi mkubwa kuliko ambao wanafanya kazi siku nzima.

Ni muda gani ulale?

Muda wa wewe kulala mchana ni mfupi sana kati ya dakika 20 mpaka 25. Hivyo hata kama unafanya kazi unaweza kutenga dakika 20 baada ya chakula na ukasinzia au kulala kidogo. Sio lazima ulale kitandani, hata kkuinamisha kichwa chako kwenye meza inakutosha kunufaika na usingizi huo. Anza sasa kujilaza dakika 20 na uboreshe maisha yako.

Nakutakia kila la kheri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment