Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, September 20, 2014

Faida Tano Za Muziki Kiafya Na Mziki Mzuri Unaoweza Kusikiliza Leo.

Watu wengi wanapenda kusikiliza mziki ili kuburudika, ila mziki una faida nyingi sana ukiacha kuburudika tu.

Mziki una faida kiafya kwa yeyote anayesikiliza. Ila mziki tunaozungumzia hapa ni mziki laini.

Zifuatazo ni faida tano za mziki kiafya.

1. Mziki husaidia hupunguza maumivu.

Watu ambao wanateseka na maumivu makali wameonesha kupata afadhali wanaposikiliza muziki laini.

2. Mziki unaimarisha kinga ya mwili.

Tafiti mbalimbali zilizofanywa na wanasayansi zinaonesha kwamba kusikiliza muziki kunaimarisha kinga ya mwili.

3. Mziki unawasaidia watoto njiti.

Watoto njiti ambao wamezaliwa kabla ya muda wa kawaida wa mtoto kuzaliwa wanaweza kunufaika sana na mziki uliopangiliwa vizuri na unaoendana na sauti zilizopo kwenye tumbo la mama.

4. Mziki unasaidia wazee.

Wazee mara nyingi hujisikia wapweke na kuwa na sononeko. Kwa kusikiliza mziki wanapata ahueni kwa kipindi kidogo.

5. Mziki unaweza kukusaidia kupunguza huzuni.

Kama una huzuni au umekasirishwa ukisikiliza mziki laini hasira zako zinaweza kupungua kwa kiasi kikubwa.

Anza kusikiliza mziki laini sasa na upate faida hizo na nyingine nyingi kiafya. Unaweza kuanza kwa kusikiliza mziki huo hapo chini.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment