Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, September 16, 2014

Sheria 10 Za Kuzingatia Kwenye Maisha.

Kuna sheria nyingi sana ambazo tunaishi nazo kwenye maisha yetu. Kuna ambazo tumezikuta kwenye jamii kwa asili na kuna ambazo zinatungwa na mamlaka husika.

Hapa kuna sheria kumi ambazo unatakiwa kuishi nazo kila siku ili kurahisisha maisha yako.

1. Ukifungua kitu, hakikisha unakifunga.

2. Ukiwasha kitu, hakikisha unakizima.

3. Ukivunja kitu, kubali umekivunja.

4. Kama huwezi kurekebisha ulichokivunja, mtafute anayeweza akirekebishe.

5. Ukikopa lipa.

 

6. Kama kuna kitu unakithamini, kijali.

7. Ukichafua, safisha.

8. Kama kitu sio chako, omba ruhusa kabla ya kukitumia.

9. Kama hujui jinsi ya kutumia kitu, jifunze kwanza au achana nacho.

10. Kama hakikuhusu usikiulizie maswali.

Kama unavyoona hizi ni sheria rahisi sana ambazo kama ukianza kuzifuata utaepukana na matatizo mengi sana. Anza kuzitumia sasa.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment