Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, September 2, 2014

NILICHOJIFUNZA LEO; Vita Kubwa Kuwahi Kutokea Afrika Ukiacha Vita Vya Pili Vya Dunia.

Ukiacha vita vya pili vya dunia vita kubwa ambayo imewahi kutokea Afrika ni vita ya pili ya Congo(Second Congo War)
Vita hii ilianza August 1998 na kutangazwa kumalizika July 2003 baada ya serikali ya mpito kushika madaraka.
congo war
Pamoja na kutangazwa kumalizika kwa vita hii bado mapigano na choko choko zinaendelea katika majimbo ya Kivu na Ituri.
Ni katika vita hii ambapo raisi wa Congo Laurent Kabila aliuawa na mtoto wake Joseph Kabila kushika madaraka ya kuongoza nchi.
Vita hii ilihusisha mataifa tisa ya Afrika na vikundi zaidi ya 20 vya wapiganaji.

Sababu ya vita hii.

Sababu kubwa iliyochangia vita hii ni mgogoro wa kimaslahi katika uchimbaji na biashara ya madini.

Madhara ya vita hii.

Vita hii ndio vita kubwa zaidi kutokea barani Afrika ukiacha vita vya pili vya dunia. Mpaka kufika mwaka 2008 zaidi ya watu milioni 5.4 walikuwa wamepoteza maisha kutokana na vita hii. Vifo vingi vilitokana na mauaji ya kuvita, huduma mbovu za afya na ukosefu wa chakula.
Kuna mengi sana ya kujifunza katika vita hii. Kwa kifupi nimeweza kukuandalia haya kwa leo.
Tukutane tena wakati mwingine. Usisahau kuweka email yako ili upate makala hizi moja kwa moja.

Vyanzo;

WIKIPEDIA; Second Congo War.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment